ASASI mbalimbali zinazojihusisha na mapambano ya udhibiti wa ugonjwa wa ukimwi, zimetakiwa kuangalia upya mipangoyao ili kuongeza nguvu zaidi ili kutokomeza maambukizi mapya ya virusi vya ugonjwa wa ukimwi
Agizo hilo limetolewa na mkuu wa mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo,kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya Ukimwi duniani Desemba mosi iliyoaadhimishwa kimkoa wilayani Longido.
Aidha amezionya asasi na mashirika
yanayotumia migongo yawagonjwa kujinufaisha na misaada inayotolewa na wahisani kuacha mara moja tabia hiyo.
’’Kuna baadhi yaasasi zimeandikishwa kufanya kazi zipo zinazotumia misaada na fedha za walengwa kujinufaisha huku walengwa wakibakia bila misaada’’alisema mulongo.
Akaziagizahalmashauri
za wilaya kufuatilia nakusimamia mipango ya mashirika hayo na kuzitaka
taasisi hizo kuhakikishazinatoa taarifa zake serikali ,wakurugenzi
afuatilie na kutambua misaada yote inayotolewa zikiwemofedha kuoana ka,a zinawafikia walengwa.
“walioanzishavituo
vya Yatima wafuatiliwe ambaowatabainika kutumia misaada hiyo ya yatima
washughulikiwe mara moja kwa kuwawanatumia migongo ya yatima
kujinufaisha na hilo halikubaliki kabisa na wala halina nafasi’aslisema, mulongo . Akaziagizahalmashauri kuwatambua waathirika ili waweze kujiunga kwenye vikundi halafu wapatiwe
mikopo kwa ajili ya
shughuli za kiuchumi,kutokana na serikali imetengamilioni 600 kwa ajili
ya kuwawezesha wagonjwa na waathirika wa ukimwi kuanzishashughuli za
kiuchumi,
Piaakazitaka halmashauri na asasi hizo kukaa pamoja na kuchambus vipaumbele katika mapambano ya ukimei kuzingatia mahitaji ya halmasauri husika’Sitaki kusikia kuna vifo tena vinavyotokana na ukosefu wa wa dawa , unyanyapaa na unyasnyasaji wowote ule ,lengolaserikali nikupunguza vifo na maambukizi nasi vinginevyo.
Mkuu wamkoa amesema kuwa hafurahishwi na kazi iliyokwisha fanywa na mashirika hayo kutokana na kuwepo ongezeko la ukimwi wakati yakidai yanatoa elimu kwa umma namna ya kupunguza maambukizi hayo
.Amesema mkoa wa Arusha una mashirika yasiyo ya kiserikali 452 ,asasi 15 licha ya kushirikiana na serikali katika mapambano hayo bado juhudi zaidi zinahitajika.
Amevikemea vyombo vya afya ambavyo vimekuwa vikivujisha siri za wagonjwa kwa
watu wasiohusika akawaagiza waratibu wa ukimwi wa ngazi zote kuanzia mkoa hadi mtaa kufuatilia ili maadili ya kitabibu yanavyotaka taarifa za wagonjwa ziwe ni siri yadumishwe.
Amesema mkoa wa Arusha una jumla ya watu 36,000katiyao ni wanawake 25,000 ambao wamejisajili
katika hosipitali, Zahanatina vituo vyaafya kwa ajili ya kuanza dawa za
kupunguza makali ya ukimwi hivyolazima tujitazame upya takwimu hizo
zinatisha.
Amewatakawanawake kuwanapotongozwa waseme haadanganyikileng nikukwepa kupata maambukizipia waliokwisha athirika wasijifiche majumbani bali wajitokeze na kujisajili ili waweze kupatiwa misaada mbalmbali.
Amesema yeyote atakaetambuliwa hatapotezamaisha yake labda kwa uweo wa
mungu tu hivyo wajitokeze wapime afya zao.
Awali akisoma taarifa afisa maendeleo ya jamii mkoa waArusha, Blandina Nkini, amesema kuwa jijila Arusha linaongoza kwa kuwa na kiwango kikubwa cha
maambukizi.
Amesema jiji la Arusha lina 5.0%likifuatiwa na wilaya ya Karatu yenye kiwango cha 3.0% Longido asilimia 2.9% Monduli ni 2.7% Arusha DC, ni 2.00% na Ngorongoro kiwango cha maambukizi ni 1.3% .
Amesema sababu kuwa ya kuongezeka kwa maambukizi hayo ni kutokana na muingiliano mkubwa wa watu wakiwemo wageni kutokana na wilaya hizo kuwa ni njia kuu ya biashara ya utalii
na madini.Amesema mkakati uliopo katika mkoa ni kuandaa kamati mpya ya
kupambana na ukimwisanjari na kuendelea na upimaji wa hiari wa afya za
wananchi katika maeneo mbalimbali.
Akawataka waliokwisha ambukizwa wasikate tama ya mnaisha na kusema kuwa mkoa unachangamoto ya kutafuta chanzo cha ongezeko hilo ambalo lilikuwa limeshashuka na ghafla limeongezzeka
Nkini, ameomngeza kuwa mkoa wa Arusha kuna watoto 6683waishio kwenye mazingira magumu na hatarishi na tayari wameshatambuliwa na kuwapatia huduma
mbalimbali kupitia kwenye mashirika na lengo ni kuwaokoa wasipate maambukizi ya ukimwi.
Amesema
jumla ya vituo 45 vimeendelea kupokea wateja na tayari watu 14151
vituonina kati yao12459 wanatumia dawa za kupunguza makali ya ukimwina
magonjwa nyemelezi. habari na Mahmoud Ahmad wa libeneke la kaskazini blog
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia