Ticker

6/recent/ticker-posts

TIMU YA WABUNGE WA TANZANIA YAAIDI USHINDI KATIKA MASHINDANO YA MABUNGE YA EAST AFRIKA YANAYOFANYIKA UGANDA



IMG_0890Timu ya WABUNGE mpira wa miguu wakifanya mazoezi katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha
IMG_0879Mwenyekiti wa timu Idd Azan akijiweka sawa kwaajili ya mazoezi
IMG_0885
IMG_0891
IMG_0894Halima Mdee ndani ya pushup
IMG_0892Timu ya wabunge mpira wa pete wakifanya mazoezi
IMG_0902TIMU YA WABUNGE  ya mpira wa miguu  imeahidi kurudi na kombe katika michuano ya kombe la mabunge la Jumuiya ya Afrika mashariki yanayotarajiwa kuanza kutimua vumbi Disemba 8 huko kampala nchini Uganda.
 
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha ambapo timu hizo za mpira wa miguu na mpira wa pete zimeweka kambi mwenyekiti wa timu Idd Azan alisema kuwa maandalizi yanakwenda vizuri na wabu nge karibu wote ambao wanaunda timu hizo wameshafika kambini tayari.
 
Kikosi hicho kilichopo chini ya kocha Kassimu Mjaliwa ambaye ni naibu waziri wa tamisemi kinaundwa na wachezaji kumi na tano ambao ni wabunge na wachezaji sita ambao ni watumishi wa bunge.
 
Azan alisema kuwa kilichopelekea kwa timu hiyo kushindwa kuchukua ubingwa ni timu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kuweka idadi kubwa ya Watumishi huku ikichezesha  wabunge sita tu ambapo kwa mwaka huu utaratibu huo umefutwa.
 
“Mwaka jana tulishindwa kuchukua ubingwa kutokana na timu uliyocheza nayo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kuchezesha watumishi wengi na idadi ya wabunge ni sita tu lakini kama wangechezesha wabunge tu ushindi ulikuwa uwe wa kwetu”alisema Azan
 
Kwa upande wake katibu wa timu hiyo Waziri Kizingiti alisema kuwa wamefurahia maandalizi na na jumla ya wanamichezo 45 lakini baada ya mazoezi wachezaji 35 wanaounda timu zote mbili wataondoka kuelekea nchini Uganda.
 
Kizingiti alisema kuwa changamoto kubwa ni muda mdogo wa mazoezi kutokana na ratiba za Wabunge lakini kutokana na mazoezi mazuri na mafundisho ya Kocha wana imanoi kuwa Kombe hilo litarudi nyumbani Tanzania.
 
Aidha aliongeza kuwa katika mechi ya Ufunguzi ambayo itachezwa tarehe 9 bunge la Tanzania itacheza na timu ya Wabunge kutoka Nchini Kenya.
 
Naye kaptein wa timu ya wanawake Grace Kiwelu alisema kuwa mazoezi yanaendelea vizuri na kila kitu kinakwenda sawa na kwamba kombe hilo bado litarudi nyumbani Tanzania.
Timu ya Bunge ya wanawake  ya mpira wa Pete ilichukua ubingwa katika mashindano yaliyopita na timu ya Wanaume ya mpira wa miguu ilichukua nafasi ya pili

Post a Comment

0 Comments