Ticker

6/recent/ticker-posts

BITEKO:WATANZANIA FICHUENI WALE WOTE WANAOKWEPA KODI NA KUTOROSHA MADINI

 
Waziri  wa  madini Doto Mashaka Biteko akipokea zawadi kutoka kwa moja wa wafanyabiashara wa madini
 Waziri  wa  madini Doto Mashaka Biteko akiongea wakati wa uzinduzi wa soko la madini mkoani Arusha lililozinduliwa rasmi leo




 baadhi ya wafanya biashara wa vito vya madini wakifatilia kwa makini

 waziri akiangalia baadhi ya vito vilivyopo katika soko hilo
 baadhi ya wafanyabiashara wakiangalia vito vilivyopo katika soko hilo



Mwenyekiti wa TAMIDA, Sammy Mollel akiongea katika uzinduzi huo ambapo alishukuru kwa kuanzishwa kwa soko la madini  pia alipongeza serikali kwa bajeti ya mwaka 2019/20 kwani  imeondoa kilio cha muda mrefu cha wachimbaji  na wauzaji wa madini nchini.



 mkuu wa wilaya ya Arusha Gabriel Daqarro akiongea katika uzinduzi huo
mbunge wa viti maalumu  ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya kudumu ya bunge nishati na madini Catherine Magige akiongea katika uzinduzi huo



Na Woinde Shizza Michuzi Tv,Arusha


Waziri  wa  madini Doto Mashaka Biteko,amewataka wafanyabishara wa madini wadogo pamoja na wakubwa kuwafichua  wafanyabiashara wote wanaojaribu kutorosha madini pamoja na wale ambao wanaokwepa kulipa kodi  ya serikali ili hatua kali zichukuliwe dhidi yao

Hayo ameyasema leo  wakati wa uzinduzi wa soko la madini mkoani Arusha ,ambapo alisema kuwa
Iwapo wafanya biashara watakuwa wawazi na watafichua watu wote ambao wanakwepa kodi na kutorosha madini hitasaidia  kwa kiasi kikubwa kukuza uchumi wa nchi yetu.

Alisema kuwa  ili kuweza kuinua uchumi wan chi yetu ni lazima kila mwananchi kutimiza wajibu wake kwa kulipa kodi  kwa uaminifu  ili kusaidia kukuza uchumi wan chi yetu aidha alisisitiza kuwa heshima kubwa ya mtanzania ni kulipa kodi na sio kufanya mambo ya kijanja janja na alibainisha kuwa ni lazima watanzania tuhame katika taifa la watu wajanja wajanja tuwe wananchi wa taifa la watu waaminifu .

“mlilalamika kuhusiana na kodi tumefanyia kazi  na yale ambayo bado tutafanyia kazi lakini kwa kuwa tumefanyia kazi na nyie rudisheni fadhila kwa kulipa kodi ,na pia napenda kuwasihi wenyeviti wa mabroka kuwakusanya mabroka ambao hawajalipa kodi kulipa kodi  wakate leseni ili nao wawe katika orodha ya walipa kodi”alisema Biteko


Alibainisha  kuwa, tangu kuingia madarakani kwa Serikali ya Awamu ya Tano, imekuwa ikisisitiza dhamira yake ya kuhakikisha Sekta ya Madini inakua, inanufaisha watanzania pamoja na kuchangia ukuaji wa Pato la Taifa


Aliendelea kueleza kuwa Serikali pia imefuta baadhi ya tozo ambazo zilikuwa kero kwa wafanyabiashara wa madini hususani wachimbaji wadogo na kufafanua kuwa tozo hizo kuwa ni pamoja na kodi ya ongezeko la thamani (VAT) asilimia 18 na kodi ya zuio ya asilimia tano kwa wachimbaji wadogo.

Alibainisha kuwa kuwekwa kwa soko hili hapa Arusha kunasaida kuwepo  kwa mazingira mazuri ya kibiashara kwenye sekta ya madini pamoja na kufuta kodi na tozo mbalimbali zinazofikia asilimia 23 na pia soko hili litasaidia kuondoa utoroshwaji wa madini na kusaidia wachimbaji wadogo kutambuliwa.

Alieleza manufaa mengine kuwa ni pamoja na kupunguza gharama za uendeshaji wa shughuli za wachimbaji wadogo na kuongeza wigo wa mapato ya nchi.

“napenda kuwasihi   wachimbaji wote wadogo na wafanyabiashara wa madini  kuendelea kushirikiana na mamlaka mbalimbali  za Serikali katika kutekeleza majukumu  yao kwa kufuata sheria, kanuni, taratibu na miongozo mbalimbali  inayotolewa na Serikali” alisema Biteko .

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo alisema kuwa manufaa ya soko jipya la madini litasaidia kuziba  mianya ambayo imekuwa chanzo cha utoroshwaji wa madini, ukwepaji kodi na hivyo kusababisha biashara nzima ya madini kufanyika kiholela katika maeneo mengi ya nchi.

Aliongeza kuwa soko hili litasaidia  kuwezesha na kurahisisha biashara nzima ya madini na kuwa kiungo muhimu cha kuwakutanisha wachimbaji na wafanyabiashara kwa lengo la kuuza na kununua madini.

aliendelea kufafanua manufaa mengine ya soko kuwa ni pamoja na kuwa suluhisho la tatizo la kupunjwa na kudhulumiwa na kuondoa  vitendo vya dhuluma ambavyo vimekuwa  vikiwahusisha wafanyabiashara wa madini wasiokuwa waaminifu kwa baadhi ya wachimbaji wadogo.

Kwa upande wake mbunge wa viti maalumu (CCM) mkoani Arusha ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya kudumu Bunge   nishati na madini  Catherine Magige alisema kuwa Soko hili litaondoa  uwezekano wa wanunuzi  wa madini kuibiwa na wajanja wachache wanaojifanya  kuwa na madini wakati hawana.

Alitumia mda huo kuwasihi  wanunuzi wa madini kulitumia soko kikamilifu ili kuepuka udanganyifu na matapeli tu








Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gamboa akiongea katika uzinduzi wa kituo cha  uuzaji madini mkoa hapa

Post a Comment

0 Comments