Ticker

6/recent/ticker-posts

SHIRIKA LA PATHFINDER LATOA MSAADA WA VIFAA TIBA VYENYETHAMANI YA ZAIDI YA MILIONI KUMI



 Meneja mradi wa shirika la PATHFINDER Amgelo Kihaga  akimkabidhi  Mkuu wa wa wilaya ya Monduli.Idd Hassan Kimanta   vifaa  tiba ikiwa ni kitanda cha upasuaji (OPERATING BED) chenye thamani ya milioni 19,mikasi na nyembe  ,Shirika hilo hilo la Parthfinder la kimataifa lililo sajiliwa hapa nchini Tanzania linalofadhiliwa na shirika la misaada la watu wa Marekani (USAID)inatekeleza miradi mbalimbali kwa miaka mitano shirika hilo linafanya kazi katika hifadhi za Taifa (TARANGIRE NATIONAL PARK ECOSYSTEM) Kwa lengo la mradi wa watu,afya,mazingira,uzazi wa mpango,cocoba na boma za mfano.


  Mkuu wa wa wilaya ya Monduli.Idd Hassan Kimanta akitoa shukrani mara baada ya kupokea   vifaa  tiba ikiwa ni kitanda cha upasuaji (OPERATING BED) chenye thamani ya milioni 19 kutoka katika shirika la Parthfinder




Woinde Shizza Globu ya jamii Arusha

 Shirika  la Parthfinder la kimataifa lililo sajiliwa hapa nchini Tanzania linalofadhiliwa na shirika la misaada la watu wa Marekani (USAID) limekabidhi vifaa tiba vyenye dhamani yilingi milioni 19,000,000 katika vituo vya afya vya wilayani Monduli.

Akikabidhi vifaa hivyo meneja mradi wa shirika hilo Angelo Kihaga alisema kuwa shirika lao linatekeleza miradi mbalimbali kwa miaka mitano pia  wanafanya  kazi katika hifadhi za Taifa za (TARANGIRE NATIONAL PARK ECOSYSTEM)  na mradi wao unalengo la kusaidi sekta mbalilimbali ikiwa ni pamoja na kusaidia watu,afya,mazingira,uzazi wa mpango,cocoba na boma za mfano.

Alisema  msaada huu ni moja  lengo lililopo katika mradi wao wa miaka mitano  ambao shirika linatekeleza ambapo alitaja baadhi ya vitu ambavyo wamevitoa kuwa ni kitanda kwa ajili ya mama kujifungulia,mikasi ,sindano ,glops pamoja na vifaa tiba vingine mbalimbali.

Kihanga alisema kuwa mradi wao wamelenga kufikia mikoa miwili ambayo ni mkoa mzima wa Arusha pamoja na Mkoa Wa Manyara pia watalenga zaidi kusaidia watu  katika sekta mbalimbali ikiwemo Afya pamoja na Mazingira

Akiongea mara baada yakupokea msaada huo mkuu wa Wilaya ya Monduli Iddi Kimanta alishukuru  shirika hilo kwa kuwa mdau mkubwa wa shughuli za maendeleo wilayani  Monduli na  kuwahaidi kuwa  atavisimamia vyema na kuvitunza ili kuweza kuendelea kuwasaidia wananchi wa wilaya hiyo hususa ni wamama wanaoenda kujifungua

Aidha mkuu huyo wa wilaya  alilitaka shirika pamoja na mashirika mengine kuendela kutoa misaada mbalimbali hususa ni katika sekta ya afya kwa ajili ya vituo vya afya vya wilaya hiyo ya monduli.

Shirika hilo hilo la Parthfinder la kimataifa lililo sajiliwa hapa nchini Tanzania linalofadhiliwa na shirika la misaada la watu wa Marekani (USAID)inatekeleza miradi mbalimbali kwa miaka mitano shirika hilo linafanya kazi katika hifadhi za Taifa (TARANGIRE NATIONAL PARK ECOSYSTEM) Kwa lengo la mradi wa watu,afya,mazingira,uzazi wa mpango,cocoba na boma za mfano.


Post a Comment

0 Comments