Ticker

6/recent/ticker-posts

NIWAJIBU WA KILA MWANANCHI KULINDA AMANI YA NCHI


Na Woinde Shizza, Arusha

Imebainika kuwa Jukumu la kulinda na kuenzi amani ambayo ni tunu kwa taifa letu ni la kil a wananchi na sio la serikali peke yake.  

Hayo yamebainishwa leo na mkuu wawilaya ya monduli Iddi kimanta akiongea na wananchi Pamoja maafisa wajeshi wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 42 tangu kuanzishwa kwa chuo hicho Pamoja na kilele cha maadhimisho ya ya miaka 54 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi la wananchi wa Tanzania sherehe zilizofanyika katika viwanja vya Polisi Wilayani Modulo. 

 Alisema kuwa niwajibu wa kila mwananchi wa Tanzania anawajibu wakulinda na kuenzi amani ya nchi yetu kama ilivyo hasisiwa na wazee wetu waliotutangulia.

Kimanta aliwapongeza jeshi kwa kazi wanazofanyaupamoja nashighuli mbalimbali mbalimbali za kijamii wanazozifa,huku akitumia muda huo kupongeza uongozi wa chuo na wanachuo wa chuo cha mafunzo ya Jeshi Monduli kwajinsi wanamahusiano mazuri baina yao na wananchi. 

Kwa upande wake kaimu mkuu wa chuo cha mafunzo ya jeshi Monduli Brigedia Je ne ra li Stephan Justice  Mnkande Alisema kuwa maadhimisho hayo yalianza rasmi August 27nayameitimishwa leo Septemba 1 ambapo alitaja shughuli zilizofanyika katika maadhimisho hayo kuwa ni Pamoja na usafi wamazingira yanayozunguka chuo, barabara ya Modulo, njia panda ya Arusha Dodoma Pamoja na utoaji wa huduma za Afya bure. 

Alisema kuwa hayo yote wamefanya ikiwa ni moja ya mahusiano bora kati ya jamii na wananchi, alisema kuwa mahusiano mazuri kati ya jamii ya watanzania ni msingi muhimu katika kudumisha undugu, urafiki na ukaribu unaoendeleza amani ya nchi yetu. 

 "napenda kuwasihi wananchi kwa ujumla kujitaidi kulinda amani yetu kwani ikipotea ningumu sana kuirejesha, tuendeleeni kuenzi amani yetu "Ali sema Mnkande. 

Aidha alitaja moja ya mafanikio waliyoyapata tangu kuanzishwa kwa chuo hicho  cha kijeshi miaka 42 iliopita kuwa ni pamoja na kuanzisha kwa kozi ya shahada ya kwanza ya sayansi ya kijeshi (bachelor Degree in Military Science) kwa kushirikiana kwa chuo cha uhasibu Arusha (AIA) iliofunguliwa november 20,2017.

Katika kilele hichi cha maadhimisho haya pia kulikuwa na michezo mbalimbali ikiwa nipamoja na maandamano ya kutembea kwa miguu kilometa nne ilioshirikisha mgeni rasmi ambaye ni mkuu wa wilaya ya Monduli, kaimu mkuu wa chuo cha kijeshi Monduli, maafisa wa jeshi Monduli, Maafisa wanafunzi wa chuo cha jeshi Monduli, wanafunzi wa Chuo cha ualimu Monduli Pamoja na wananchi wa monduli

Aidha pia kulikuwa na michezo mingine kama mpira wa miguu, kukimbiza kuku kuvuta kamba pamoja na mazoezi ya mwili (arabicki





 
 mkuu wawilaya ya Monduli Iddi kimanta akiwa anabadilishana mawazo na kaimu mkuu wa chuo cha Mafunzo ya kijeshi Monduli Brigedia Jenerali Stephen Justice Mnkande wakati wa maathimisho ya miaka 54 tangu kuanzishwa kwa chuo chamafunzo ya kijeshi na miaka 42 tangu kuasisiwa kwake monduli
 kaimu mkuu wa chuo cha mafunzo ya jeshi Monduli Brigedia Je ne ra li Stephan Justice  Mnkande akiongea katika maadhimisho hayo
 Mkuu wa wilaya Monduli na kaimu mkuu wa chuo cha kijeshi monduli wakiwa katika matembezi ya kilometa nne



 

Post a Comment

0 Comments