Ticker

6/recent/ticker-posts

RC ALLY HAPI:MAJENGO YA UWANJA WA NDEGE WA NDULI YANAHARIBU TASWIRA YA KUIJENGA IRINGA MPYA


Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi akiwa ameongozana na mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela pamoja na meneja wa uwanja wa nduli Anna Kibopile alipofanya ziara katika uwanja wa ndege wa Nduli kwa kufahamu maendeleo ya ukarabati mdogo wa uwanja huo na kubaini baadahi ya changamoto zinaukabili uwanja huo hasa katika swala la majengo kuto kidhi mahitaji ya wasafiri 
Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi akiwa ameongozana na mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela pamoja na meneja wa uwanja wa nduli Anna Kibopile wakiwa kwenye eneo ambalo linafanyiwa ukarabati mdogo 
 Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi akiwa ameongozana na mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela wakipata maelezo kutoka kwa meneja wa uwanja wa nduli Anna Kibopile juu ya ukarabati wa uwanja unaoendelea

Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi akiwa ameongozana na mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela pamoja na kamanda wa police mkoa wa Iringa Juma Bwire wakiangalia jengo la wasafiri katika uwanja wa nduli mkoani Iringa
Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi akiwa ameongozana na mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela pamoja na meneja wa uwanja wa nduli Anna Kibopile wakiwa ndani katika sehemu ya abiri ambao wanasubiri kusafiri.  
Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi akiongea na waandishi wa habari wakati wa ziara katika uwanja wa nduli na kubaini mapungufu mengi ikiwapo gari hilo ambalo linaonekana la zimamoto ambalo toka lifike hapo halijawi kufanya kazi kutokana na kuwa bovu na spea zake kutopatikana.

NA FREDY MGUNDA,IRINGA.

MKUU wa mkoa wa Iringa Ally Hapi hajaridhishwa na hali halisi ya uwanja wa ndege wa nduli uliopo kata ya nduli kuelekea kuijenga Iringa mpya kwa maendeleo ya wanairinga.

Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua ukarabati mdogo unaoendelea katika uwanja huo,hapi alisema kuwa uwanja huo wa ndege unahitaji ukarabati wa maana ili kukidhi mahitaji ya watumiaji na kukuza maendeleo ya wananchi wa mkoa wa Iringa.

“Nimetembea kwenye maeneo mengi ya uwanja huu hayaridhi wala hayavutii kwa wawekezaji kuja mkoani hapa kwa kuwa saizi wawekezaji wengi wanapenda kutumia usafiri wa anga hivyo ni lazima kuwa na kiwanja cha ndege ambacho kitakidhi na kuvutia watalii na wawekezaji wanapokuja mkoani hapa” alisema Hapi

Hapi alisema kuwa jengo la wageni la uwanja huo ni dogo,halina ubora unaotakiwa na halikidhi kuwa katika uwanja huo ambao hivi karibuni utaanza kupokea wageni wengi kutoka maeneo mbalimbali ya ndani ya nje ya nchi.

“Sehemu hii ya kupumzikia wageni hakuna,sehemu ya wasafiri wanapoongokea bado ni ndogo na haina vigezo vya kuwa eneo la kupuzikia wasafiri,vyoo havifai eneo lenyewe bado halina miundombinu ya kisasa ambayo itawavutia watu wengi kuja mkoani Iringa hivyo tunahitaji kujenga jengo jipya na la kisasa kabisa” alisema Hapi

Haiwezekani uwanja wa ndegehuu  ukawa unamajengo na vifaa vingi ambavyo vimechoka na havikizi mahitaji ya kuijenga Iringa mpya hivyo ni lazima kuwekeza kwenye uwanja ili kuvutia wawekezaji na watalii ambao watakuja mkoani hapa.

Hapi aliongeza kuwa uwanja wa ndege wa Nduli hauna hapa gari la fire ambalo litasaidia kuongoa majanga yoyote yatakayotokea kwenye uwanja huu,hivyo ni lazima tserikali ijue kuwa tunahitaji kuwa na gari la fire hapa kwa kuwa Iringa ni kitovu cha utali nyanda za juu kusini.

“Nimejionea hapa mwenyewe kuwa hakuna gari la fire linalofanya kazi kwa kuwa lililopo ni bovu na haliwezi kutengenezeka kwa kuwa liltengenezwa kwenye viwanda vya miaka mingi iliyopita na spea zake hazipatika hata nje ya nchi kwa mjibu wa wataalamu ambao wamenieleza hapa” alisema Hapi

Hapi alisema kuwa gari ambalo lipo katika uwanja wa ndege wa Nduli halijawahi kufanya kazi toka liletwe na inasadikiaka kuwa litengenezwa miaka ya themanini huko hivyo hakuna gari la zimamoto katika eneo hili  hivyo ni hatari kwa watumiaji wa uwanja huu.

Aidha hapa alisema kuwa uwanja wa ndege wa Nduli unaumuhimu mkubwa wa kukuza uchumi wa mkoa wa Iringa kwa kuwa watalii na wawekezaji wengi watautumia uwanja huu wa ndege kufanya kazi kwa muda muafaka na kurudi walikotoka kwa kutumia usafiri wa anga.

“Ukiwa na uwanja wa ndege ambao unakidhi vigezo vinavyotakiwa utasaidia kuongeza utalii wa kusini kama ambavyo unajua kuwa Iringa ndio kitovu cha utalii na kuvutia wawekezaji wengi ambao mara nyingi wamekuwa wakitumia usafiri wa anga tofautia wachache ambao wamekuwa wakitumia usafiri wa barabara za chini” alisema Hapi

Naye meneja wa uwanja wa ndege wa Nduli Anna Kibopile alisema kuwa jengo la abiria halikidhi mahitaji kupokea abiri wengi ambao pia watakuwa wakitumia ndege ya serikali aina ya Bombardie ambayo itaanza safari mkoani Iringa hapo baadae.

“Unajua kuwa ndege yetu ya Bombardie ataanza safari ya kuja hapa mkoani hiyo itakuwa inachukua abiria wengi sana hivyo jengo letu la abiria halitoshi kuwahudumia wasafiri ambao watakuwa wakiutumia unjwa huo kufanya safari zao” alisema Kibopile

Kibopile  alisema kuwa ndege ya Bombardie inabeba abira zaidi ya sabini hivyo ni lazima kuhakikisha tunataua au tunajenga jengo kubwa la abira ambalo mkuu wa mkoa wa iringa ameshauri kuwa jengo hilo halikidhi mahitaji ya abiria ambao watakaokuwa wanakuja mkoani Iringa.

Post a Comment

0 Comments