KILIMO CHA MBOGA NA MATUNDA (HORTICULTURE)KINAVYOWEZA KUMTOA MWANAMKE KATIKA UMASKINI
NA WOINDE SHIZZA,ARUSHA
- 'ushiriki wa wanawake kwenye Kilimo
nchini Tanzania kwa takwimu za mwaka 2003 ni asilimia ni 54%.
-
Kwa ujumla Wanawake asilimia 81% wanafanya
shughuli mbalimbali zinazo husiana na
kilimo.
-
Tasnia ya horticulture inayo husisha
mazao ya Mbogamboga na matunda ni moja ya sekta ndogo inayo kuwa kwa kasi sana
nchini kufikia ukuaji wa asili 8 mpaka 9 kufikia mwaka 2021, huku ikiwa ni sekta
inayoingizia mapato serikali kwa wingi kuliko zingine katika sekta ya Kilimo.
Irene Mollel ni msichana ambaye ameweza kujikwamua kiuchumi kupitia kilimo cha na maua ,mboga,matunda ,mimea
itokanayo na mizizi na viungo (horticulture) ,kitu ambacho kilimvutia
alipotembelea moja ya maonyesho ya nane nane yaliyowahi kufanyika mkoani
Arusha na sasa ni mkulima mzuri na mkubwa wa kilimo cha nyanya.
Alisema kuwa aliaangalia kilimo cha nyanya ,vitunguu na vingine alipotembelea maonyesho
ya nane nane ambapo alivutiwa zaidi alipotembelea banda la Asasi kilele ya sekta binafsi inayojishughulisha
na kuendeleza kilimo cha horticulture
nchini kwa mazao kama maua ,mboga,matunda ,mimea itokanayo na mizizi na viungo
TAHA.
Alisema kuwa kabla ya kufika katika maonyesho hayo na
kujionea fursa hiyo ya kilimo
alishajaribu kulima lakini hakufanikiwa na alikata tamaa lakini wakati
akiendelea kutembelea ,mitandao ya kijamii
na alipofika katika ukurasa wa
kijamii wa asasi ya Taha Instagram
aliona tangazo la fursa ya vijana
kusapotiwa na aliamua kujiunga na kuanza
kilimo rasmi.
KUANZA KWAKE MAFUNZO
RASMI
Irene Mollel alisema kuwa alianza kupata mafunzo kutoka kwa
bwana shamba na alianza kufundishwa
kilimo cha matone (drip eligetion system)namna ya kusia mbegu kwenye vitalu kwa kutumia treyi ,ambapo pia alimuandalia ratiba nzuri ya kuweka
mbolea ya kisasa aina tofauti tofauti katika nyanya zake mbali na hili alikuwa akitembelewa na
kushauriwa namna ya kusafisha shamba mara kwa mara na mwalimu wake ambaye ni
Bwana shamba
Ambapo Bwana shamba huyo kumtembelea katika hatua za mwanzo
za kilimo cha nyaya na kumpa ushauri wa
mambo mbalimbali kumemsaidia sana hali iliompelekea kupata mazao mengi na yenye ubora.
AMENUFAIKAJE KWA UPANDE WA MASOKO
Anaenda mbali zaidi na
kubainisha kuwa kwa upande wa masoko
amenufaika Kwa sababu ameweza kupewa muongozo kutoka Taha amelima kwa
wakati ambao bidhaa inanunulika Kwa bei nzuri ambayo inamuwezesha mkulima
"Kwaiyo wateja wametufata hapa hapa shambani wamenunua
kwa bei nzuri ambayo ni rafiki kwa mkulima na pia kwa mteja niende ndani
zaidi kipindi kilichopita
nilipoanza nililima hekari moja lakini sikupata kitu maana sikuwa na elimu lakini
kipindi kilichofuata nimelima
hekari hiyo hiyo moja nani nimepata
mazao mengi ambayo yamenisaidia kuongeza mtaji
wangu wa kilimo" alisema
KIPATO ANACHOKIPATA ANATARAJIA KUFANYIA NINI
Irene anasema kuwa kutokana na kipato anachokipata kila msimu anapenda kuongeza ekari zingine
mbili pamoja na kuongeza idadi ya wafanyakazi
watakao msaidia kufanya kazi kwa
ufanisi zaidi ili aendelee kuwa mfanyabiashara mkubwa zaidi
Aliishukuru sana TAHA pamoja na wania wake kwa kumuwezesha
kupata mtaji ,elimu ya kilimo cha horticulture
pamoja na kumfundisha namna gani
ataweza kulima na kupata fedha za kuendesha maisha yake
Irene amewataka wanawake kuacha woga wa Kujiingiza kwenye
kilimo ,kwani kilimo cha horticulture ni kizuri na pia kinalipa
Aliwataka wanawake
wale wanaolima kuacha kufanya kilimo cha mazoea kama vile cha kutegemea mvua badala
yake waingie katika kilimo cha
horticulture ambacho unaweza kutumia mbinu mbalimbali za umwagiliaji wa kisasa.
Anaeleza kuwa alikaa nyumbani kwa kipindi cha muda mrefu kidogo baada ya hapo akaamua kujiingiza
katika kilimo katika shamba lake la ekari 1 mwaka 2018 akiwa na ujuzi mdogo wa
uzalishaji na upatikanaji wa masoko uliopelekea
kusababisha mazao kuharibika shambani kutokana na kile kialichodai
kukosa masoko ya uhakika
Anaeleza kuwa alijiunga na huduma za Tanzania Horticultural
Association
Eva anaenda mbali Zaidi na kubainisha kuwa soko la
mazao yake analipata katika masoko ya Dar es Salaam, Dodoma, Morogoro na
awali alikuwa akiuza Kenya kabla ya
kuzuka kwa Covid - 19.
“Sasa hivi natarajia
kuvuna ekari 5 za mananasi na napia natarajia faida ya zaidi ya shilingi za
kitanzania milioni kumi ( 10), pia
kupitia kilimo hichihichi cha horticulture nimeweza kuipatia familia yangu
mahitaji ya msingi kama kujenga nyumba yangu
na pia kuwajengea wazazi wangu, nimejenga fremu za maduka ya kukodisha na naninasaidia
wanafunzi 13 kwenye eneo ninaloishi
mahitaji ya shule ili waweze kutimiza ndoto zao na wasiishie njiani kama
mimi”
Eva John anawasihi wanawake kutokata tamaa hata kama wamefeli
au wameshidwa kuendelea na masomo yao wanaweza wakajiwekeza katika kilimo cha
hotculture maana kina lipa na kinafaida kuliko kukaa bila kufanya kazi au
kulima kilimo cha mazoea
Alisema kuwa fursa ni nyingi sana za kilimo cha mazao haya lakini
wanawake wengi wamekuwa wakijachwa nyuma ,na kuacha kuzikimbilia hivyo aliwataka
waamke na waanze kuzikimbilia fursa hizi huku akibainisha kuwa masoko yapo ila
tatizo kubwa ni uchache wa wanawake wanaoshiriki katika mnyororo mzima wa mazao
ya horticulture.
“wanawake wengi wamekuwa wanalalamika ajira hazipatikani wakati yapo maeneo mengi ya
ukezaji ambayo yanaweza kumkomboa mwanamke kiuchumi na niseme fursa ni nyingi sana za mazao “
Alikazia Dkt. Mkindi.
Mnyororo huu hauishii hapo lakini kuna maeneo kama ya uuzaji
wa miche, na kutengeneza bustani za maua mbalimbali ambazo zitawaingizia
kipato,
Aidha aliongeza mazao ya Horticulture kutoka Tanzania yamekua
na mwitikio mzuri kutokanna kukua kwa soko katika masoko ya nchi za Afrika Mashariki pamoja na nchi za kusini mwa Afrika hivyo ni
vyema wanawake wakaanza kuwekeza kwenye
kilimo maana kilimo kina lipa .


I like how you educate us woinde
ReplyDelete