Ticker

6/recent/ticker-posts

WATANZANIA WATAKIWA KUJENGA TABIA YA KUPIMA AFYA ZAO MARA KWA MARA



Mtaalamu wa kutibu magonjwa mbalimbali ya binadamu Kwa tiba asili  ambaye pia ni Mkurugenzi  wa kazoba international herbal products Dkt Mwasiga Kazoba akitoa maelekezo Kwa wateja wake ambao ni wagonjwa waliofika ofisini kwake zilizopo ndani ya halmashauri ya Jiji la Arusha   namna dawa zake za asili zinavyofanya kazi

 Na Woinde Shizza,Arusha

Katika ulimwengu wa leo unaohitaji nguvu katika  kazi na biashara, baadhi ya watanzania wamebainika  kutokuwa na utamaduni wa  kupima  afya zao mara kwa mara  na kusahau kuwa Kupima afya kunaweza kuokoa maisha na kuzuia matatizo yanayoweza kuepukika.

 

Hayo yamebainishwa na mtaalamu wa kutibu magonjwa mbalimbali ya binadamu kwa tiba asili  ambaye pia ni Mkurugenzi  wa kazoba international herbal products Dkt Mwasiga Kazoba wakati akiongea na waandishi wa habari ambapo alisema kuwa watanzania wengi wamekuwa na tabia ya kutokujua hali yao  ya afya jambo ambalo linaweza kuwa kuwa hatari kwao.

 


Alisema kuwa anapenda kuwahimiza  watanzania kuweka umuhimu sawa kati ya majukumu yao ya kila siku na kutunza afya zao kwa kufanya uchunguzi wa mara kwa mara kwani ni njia nzuri ya kutambua mapema matatizo yanayoweza kujitokeza na kuchukua hatua mapema.

 

‘’Kubadilisha mtazamo wetu kuhusu afya ni muhimu,afya siyo tu kujisikia vizuri leo, bali ni uwekezaji wa maisha marefu na yenye furaha ,tushirikiane katika kuhamasisha wenzetu, marafiki, na familia kufanya uchunguzi wa afya,ili tuweze kujenga jamii yenye nguvu na afya bora’’alisema Dkt Kizoba

 

Alisema kuwa ni wakati wa kila mmoja wetu kumuhamasisha  mwenzake kuwa na tabia ya kufanya uchunguzi wa  afya na swala hili  kuwa sehemu ya maisha yake  ya kila siku

‘’Tuanze kufanya maamuzi mazuri kwa afya zetu, tukitambua kuwa afya yetu ni mali  Kwa kufanya hivyo, tutajenga jamii yenye uelewa wa kina wa umuhimu wa kupima afya mara kwa mara”alibainisha Dkt Kizoba

Aidha alimtaka kila mtanzania kumuhimiza mwenzake  kufanya mazoea ya kupima afya, kwa kushirikiana na taasisi za afya kutoa elimu, na kuondoa vizuizi vinavyoweza kuzuia watu kufanya uchunguzi,huku akisisitiza kuwa  Kupima afya isiwe ni jambo la dharura tu, bali iwe ni mtindo wa Maisha kwa kila mt una kwa pamoja, wafanye swala la kuchunguza afya kuwa sehemu ya utamaduni wao wa kila siku kwani  wakiimarisha jamii yenye afya, furaha, na maendeleo.

Aliongeza kuwa Watanzania wanatakiwa kutambua kuwa afya zao  ndio mitaji  yao  mikubwa hivyo wametakiwa  kujenga tabia ya kufanya uchunguzi wa mara kwa mara ya miili yao ili kuepuka matatizo makubwa ya kiafya huku akisisitiza kauli mbiu  yao ya kizoba kuzingatiwa inayosema ‘afya yako ndio mtaji wako wa kwanza.

Post a Comment

0 Comments