Ticker

6/recent/ticker-posts

TWASIRA YA MAHAFALI YA TANO YA CHUO CHA UFUNDI ARUSHA



Mgeni Rasmi, Naibu Waziri wa Elimu, Mh. Philipo Mulugo akihutubia wahitimu na wageni waalikwa kwenye Mahafali ya Tano ya Chuo cha Ufundi Arusha (ATC).
Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Ufundi Arusha, Bw. Abraham Nyanda akitoa Hotuba wakati wa Mahafali.
Mkuu wa Chuo cha Ufundi, Eng. Dkt. Richard Masika akitoa Hotuba wakati wa Mahafali ya Tano ya Chuo.
Wafunzi bora Kumi (10) wakiwa wameshikilia Mfano wa Hundi ya Sh. Mil 10 wakiwa katika picha ya Pamoja na Mgeni Rasmi Naibu waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mh. Philipo Mulugo pamoja na baadhi ya Wageni Waalikwa. Fedha hizi ni Ahadi ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Mizengo Peter Pinda (MB) kwenye mahali ya Nne na Tano. 
  Chuo cha Ufundi Arusha (ATC) kimedhamiria kutumia wanafunzi pamoja na wakufunzi wao kubuni teknolojia rahisi itakayoweza kumaliza tatizo la umeme maeneo ya vijijini.

Pamoja na jukumu la kuzalisha wataalamu wa fani mbalimbali, taasisi za elimu nchini zina nafasi kubwa ya kutatua changamoto kadhaa zinazolikabili taifa hili.
Kwa mfano, Chuo cha Ufundi Arusha (ATC) kimedhamiria kutumia wanafunzi pamoja na wakufunzi wao kubuni teknolojia rahisi itakayoweza kumaliza tatizo la umeme maeneo ya vijijini.
Mhandisi Urbanus Melkior, ni Mkuu wa Idara ya Umeme chuoni hapo, anayeamini kuwa wanafunzi wao kwa kushirikiana na wakufunzi, wanaweza kusaidia kutatua tatizo la umeme vijijini.
Katika kutekeleza hilo, anasema chuo hicho kimebuni mtambo mdogo wa kufua umeme ujulikanao kwa Kiingereza ‘Mini hydro Turbines’, unaotumia maji kwa kiasi kidogo.
“Mwaka 2011 kulikuwa na mgao mkubwa wa umeme. Watu walikuwa wanakaa bila umeme kwa kati ya saa nane mpaka 11, hali hiyo ilitufanya tufikiri jinsi tutakavyoweza kufanya, ili kupata ufumbuzi wa tatizo la umeme,” anasema.
Anaeleza kuwa, baada ya hapo idara ya umeme ilishirikiana na idara ya mitambo hatimaye walifanikiwa kutengeza mtambo huo ambao umefungwa katika eneo la Makumira wilayani Arumeru.
Melkior anasema kwamba, mtambo huo unaweza kuzalisha umeme kwa kutumia maji kidogo yanayopita kwenye mfereji. Kwa sasa takriban kaya 20 zinahudumiwa na umeme huo.
“Tunachofanya sisi ni kutengeneza mtambo na kwenda kuufunga, tukimaliza tunawaachia wanakijiji wanaoutunza,” anasema.
Anaeleza kuwa, teknolojia iliyotumika kuutengeza ni rahisi na inaruhusu mtu yeyote hata asiyekuwa mtaalamu wa umeme kuweza kuuhudumia mtambo huo.
“Mtambo ukishawekwa, kazi itakayokuwa inafanyika ni kufungulia maji yaje kwenye mtambo ama kuyapunguza, nyingine ni kupaka vilainishi tu, hii anaweza kufanya mtu yeyote,” anaeleza.
Mbali ya Makumira, mtambo huo pia umefungwa katika maeneo mbalimbali ya mikoa ya Morogoro, Iringa , Katavi, Njombe na Ruvuma.
 

Post a Comment

0 Comments