Ticker

6/recent/ticker-posts

WAIPONGEZA KAMATI KUU KWA KUMPITISHA DKT.TULIA


 


Na mwandishi wetu

Mjumbe wa halmashauri kuu ya Taifa wa CCM Taifa(MNEC) William Sarakikya
ameipongeza Kamati Kuu ya CCM chini ya Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa kumteua Dr Tulia Ackson Mwansasu kuwa mgombea nafasi ya Uspika katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi.


Alisema kuwa tulia  ana sifa, uwezo, uzoefu na amedhihirisha uwezo wa kumudu changamoto za kuliongoza Bunge kwa weledi, umahiri na ufanisi. 


Alisema kuwa ni vyema  wana CCM na Watanzania wote kuungana na kamati kuu ya CCM kwenye uteuzi huu ili kuhakikisha bunge  linapata Spika atakayeweza kusimamia utekelezaji kikamilifu wa  majukumu ya Bunge


Aidha pia alisema kuwa Dr.Tulia anaweza   kuishauri serikali jinsi ya kukabiliana na changamoto za sasa hivi kwani ni mzoefu wa kuendesha bunge  Kwa muda mrefu.




Post a Comment

0 Comments