Akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam leo tarehe 22.01.2025 Mkurugenzi wa Elimu kwa Mlipakodi na Mawasiliano wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Richard Kayombo amesema zawadi hizo zitatolewa kwa Walipakodi waliyofanya vizuri katika kulipa Kodi kwa kipindi cha Julai 2023 mpaka June 2024.
Kayombo ametaja vigezo walivyotumia kuwachagua wanaopewa zawadi ikiwemo Mlipakodi kodi mwenye rekodi nzuri katika ulipaji wa Kodi, Mlipakodi kwa hiari na kwa wakati, Mlipakodi anayetumia EFD mashine kikamilifu, Mlipakodi aliyelipa kodi kubwa zaidi na Mlipakodi anayetoa ushirikiano kwa TRA.
Kayombo amesema zawadi hizo zitachagiza Walipakodi wengine kufanya vizuri zaidi ili na wao watunukiwe wakati ujao.
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia