TEMDO YAJA NA SULUHISHO LA SUMU KUVU KATIKA ZAO LA MIHOGO

Afisa wa Kitengo cha Mawasiliano na Masoko Dkt. Sigisbert Mmasi kutoka Taasisi ya ubunifu na Usanifu mitambi Tanzania (TEMDO)akitoa maelezo  Kwa naibu Katibu Mkuu wa wizara ya uwekezaji ,viwanja na biashara Ally Gugu  pamoja  baadhi ya wananchi waliotembelea  banda lao lililopo katika maonyesho ya 17 ya SIDO Kanda ya kaskazini yanayofanyika katika viwanja vya makumbusho vilivyopo ndani ya halmashauri ya jiji la Arusha mkoani Arusha

 Na Woinde Shizza,Arusha

 Tatizo  la kumaliza  uwepo wa sumu kuvu katika zao la muhogo limepatiwa ufumbuzi na  Taasisi ya Uhandisi na Usanifu  Mitambo Tanzania (TEMDO)  mara baada ya kuwabunia wakulima wa zao hiyo mtambo utakao wasaidia  kuchakata  zao hilo   mara tu baada ya   kuvunwa .

 

Hayo yamebainishwa na Ofisa wa kitengo cha Mawasiliano na Masoko Dkt. Sigisbert Mmasi kutoka Taasisi ya ubunifu na Usanifu mitambi Tanzania (TEMDO) wakati akiongea katika  maonyesho ya 17 ya SIDO Kanda ya kaskazini yanayofanyika katika viwanja vya makumbusho vilivyopo ndani ya halmashauri ya jiji la Arusha mkoani Arusha  ambapo alisema kuwa mashine hiyo itamkomboa sana mkulima wa zao la muogo

 

 

Alisema kuwa Mtambo huu utakuwa mkombozi  kwa wakulima kwakuwa   muhogo ukivunwa unatakiwa  uchakatwe mapema maana ukikaa sana unaweza ukaharibika ,ukatengeneza sumu kuvu ambayo ni  Kuvu/ukungu/fangasi hushambulia mazao mbalimbali ya chakula, ambapo kawaida kuvu hupatikana kwenye udongo wakati wote katika hali ya vumbi  au muhogo huo  ukaharibika ukawa haufai tena kwa matumizi ya  binadamu

 

 

Alibainisha kuwa  temdo kila mwaka wanakuja na kitu kipya ambacho kitamsaidia mkulima  katika kazi  zake pamoja na kutatua matatizo  katika kilimo anachofanya  ,na kwa mwaka huu wameamua kumletea mkulima mtambo huo ambao utamsaidia mkulima kuokoa mazao yake ambayo yalikuwa yakiaribika   kutokana na kukosa soko

 

Alisema kuwa mtambo huo  unauwezo wa kuchakata zao la muhogo takribani tani 12  na wenyewe unakuwa na tani elfu 12000 za muhogo ambapo ukichakata unapata unga takribani  tani  tatu.

“mtambo huu ni wa kisasa na unamsaidia mkulima kwa sababu unauwezo wa kuvuna muhogo siku hiyo hiyo na  kuchakata siku hiyo hiyo  ,na niwaambie ukishavuna muhogo wako unaumenya unaingiza kwenye mashine  unatengenezwa uji baada ya  apo  unawekwa kwenye draya  ambayo inasaidia kukausha ule unga wa muhogo siku hiyo hiyo kwa iyo unapata unga siku hiyo hiyo ,na unaweza kupeleka kwa walaji siku hiyo hiyo“alibainisha Mmasi

 Alisema kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa ya kutokuwa na mvua  kwa kipindi kirefu  mtambo huo utasaidia kuokoa kile chakula ambacho kilikuwa kinapotea kwa kuoza bure  kutokana na kukaa mda mrefu bila kuchakatwa .

 

 

 

 

 

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

إرسال تعليق

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia