ZIJUE BAADHI YA SABABU ZINAZOSABABISHA UGUMBA KWA MWANAMKE

'tatizo la ndoa nyingi kuvunjika na wanawake  kukosa watoto,linaongezeka kadri siku zinavyozidi  kwenda.


Tatizo la   Ndoa nyingi kuvunjika  na  wanawake kukosa watoto, linaongezeka kadri  siku zinavyozidi kwenda  ,  watu mbalimbali   wanaelezea baadhi ya sababu  zinazofanya watu hao kukosa  watoto huku wengine wakisema ni vyakula vinavyoliwa na wanawake kwa kipindi hichi  huku baadhi wakibainisha ni wasichana au wanawake   kutoa mimba , kutumia madawa ya uzazi  wa mpango angali bado mabinti wadogo .

 

utafiti unaonyesha katika kila ndoa tano au mahusiano matano ya kimapenzi basi uhusiano mmoja una matatizo ya uzazi hasa ya kushindwa kuzaa. 

 

 

hali hii imekua ikiongezeka kadri miaka inavyozidi  kwenda  mbele kwa sababu mbalimbali kama mionzi ya mawasiliano yaani wi-fi , magonjwa mapya ya binadamu  kwa wanawake utafiti mpya unasema uwezo wao wa kubeba mimba unaanza kupungua baada ya miaka 30 ya umri kutokana na kuanza kuishiwa nguvu kwa viungo vya uzazi.

 

 


Rose Roberty (change Muja) ni mwanamke ambaye anajishughulisha na utoaji wa dawa za miti shamba kwa wanawake pamoja na dawa zingine mbalimbali    akionyesha  Moja ya dawa anayotoa

 

Mwanamama mmoja ambaye anatoa dawa za asili za uzazi pamoja na zingine anaelezea baadhi ya sababu zinazofanya  wanawake wengi kukosa watoto ambapo anafafanua kuwa  moja wapo ya sababu  ni pamoja na kutumia madawa ya uzazi wa mpango katika umri mdogo

 

 

Rose Roberty (change Muja) ni mwanamke ambaye anajishughulisha na utoaji wa dawa za miti shamba kwa wanawake pamoja na dawa zingine mbalimbali   anaeleza sababu kubwa zinazofanya wanawake wengi kutopata watoto  wanapoingia katika ndoa au wanapofikia katika kipindi cha kutafuta  mtoto

 

-Ulaji wa madawa ya uzazi wa mpango

Rose Roberty (change Muja) anasema kuwa kwa kipindi cha sasa hivi wasichana wengi wanajiingiza katika swala la kufanya ngono nje ya ndoa hali ambayo inawapelekea kujiingiza  katika matumizi ya dawa za uzazi wa mpango kabla ya muda wake

 

‘’mimi na tembelewa na wanawake wengi wakiwa wanatafuta watoto unakuta mtu amekaa kwenye ndoa mwaka ajapata mtoto  anakuja kunywa dawa hizi za miti shamba  baadhi yao wanabahatika wanapata na baadhi hawapati lakini ukifuata historia yao ya nyumba  unawapo wauliza wengi wao wanadai walikuwa wanatumia vidonge vya uzazi wa mpango mara tu walipoanza sekondari “

 

“wanasema kuwa imewalazimu kutumia kutokana na kujiingiza katika tendo la ndoa  kipindi wakiwa na umri mdogo sana, na  wengine ukifuatilia historia yao  wanakwambia walitoa mimba walivyokuwa shuleni   ,

 

Anasema kwa sasa mfano binti anamiaka 15 anaenda kutoa mimba kwakweli wengine wanatumia njia salama ambayo ni hospitali huku wengine wakitumia njia za asili

 

Anabainisha kuwa hata njia ya hospitali ya utoaji wa mimba katika umri mdogo nayo niseme tu sio ya uhakika sana maana katika kuchokonolowa unaweza kuguswa kizazi na ndio kikaharibika kabisa hali ambayo inamfanya mwanamke huyo ata akiingia kwenye ndoa kushidwa kubeba mimba

 

 


-kujiingiza mahusiano ya ngono wakiwa wadogo

 Anaenda mbali na kubainisha  katika kipichi cha zamani watoto wa kike, walikuwa hawajiingizi katika matendo ya ngono katika umri mdogo lakini kwa kipindi cha sasa wanawake wengi wamekuwa wakijiingiza katika   matendo hayo, wakiwa na umri mdogo hali ambayo inapelekea kizazi  kuanza kusumbuliwa kikiwa bado hakija komaa vyema 

 

“nitoe mfano tu wa hawa mabinti zetu kwakweli  wanavyoanza kufanya mapenzi wakiwa wadogo unakuta mtoto wa miaka 13 anatembea na mbaba wa miaka 30 kweli apo ndugu mwandishi hata ukiangalia wanaendana   sindo akimuingilia uyu mwanamke sindio anasogeza kizazi kabisa  sasa apo ndio kamfanya  mpenzi wake akishatumika vya kutosha hadi anafikia umri wa kuolewa si anakuta kizazi kimeisha hakipo karibu kabisa   ndio wanakuja kutafuta watoto hapo baadae mpaka wanafukuzwa kwenye ndoa,  alafu wanaanza kulalamika  bure kuwa wamelogwa au ni MUNGU, wewe angalia tu wanaokimbilia kwenye makanisa ukichunguza historia zao utashangaa”

 

ATOA USHAURI

Aidha  Bi.Rose aliwashauri wasichana ambao ni wanawake kuacha kutumia vidonge vya uzazi wampango  kabla hawaja zaa   au kabla ya kufikia kipindi chake kwani kufanya hivyo kutawaletea madhara makubwa sana hapo baada

 

Aliongeza kuwa pia ni vyema wakaacha kutoa mimba haswa katika kipindi wanapo kuwa  na umri mdogo kwani wengi wao ndio wanapoelekea kupata matatizo  ya kukosa mtoto ,ambapo pia aliwataka kuacha kuwa  na tamaa ambazo ndio zinawapelekea  kutembea na watu waliowazidi mri ambao baada ya kufanya nao mapenzi wanawaharibu na kuwasababishia matatizo hapo baada.

 

MTAALAMU WA AFYA AELEZEA VYEMA NINI MAANA YA UGUMBA

Brenda Charles ni muuguzi wa kituo cha afya cha Kaloleni aelezea nini maana halisi ya  ugumba  nanini kinasababisha 

 

-Ugumba ni nini

 Hii ni hali ya wapenzi au mke na mume kutopata ujauzito baada ya kushiriki tendo la ndoa bila  kutumia kinga kwa muda wa mwaka mmoja mfululizo.

-Aina za ugumba 

 unaweza kua wa aina mbili ya kwanza ni ile ijulikanayo kama  primary infertility yaani mtu hajawahi kubeba mimba kabisa   tangu azaliwe  na ya pili ni secondary infertility  hii ni ile ya mtu ambaye amewahi kuzaa lakini kwa sasa ameshindwa kubeba ujauzito.

 

Aidha ugumba una vyanzo vingi  ambavyo vingine havifahamiki mpaka   lakini  ngoja niwaeleze baadhi ya vyanzo hivyo.

 

 

·     utoaji wa mimba

Huenda hichi ndio kitakua chanzo kikuu cha ugumba miaka ijayo kwani siku hizi kila karibia kila mwanamke ana sababu za kutoa mimba, utoaji wa mimba una hatari nyingi ambazo huweza kuleta ugumba kama kuoza au kuharibika kwa kizazi baada ya kushambuliwa na bakteria, makovu yanayoletwa na vifaa vinavyotumika kutoa mimba kwenye mfuko wa uzazi na mlango wa uzazi huweza kusababisha ugumba usiotibika.

 

·     matatizo ya vizaalishaji vya mayai [ovari]

 ovari ni kiungo ambacho kinatoa yai moja kila mwezi ili liweze kurutubishwa na mbegu ya mwanaume lakini kuna magonjwa ambayo yanaweza kusababisha ovari hiyo ikaugua na kushindwa kutoa mayai, mwanamke ana ovari mbili lakini moja ikiuugua tu na nyingine haifanyi kazi mfano ugonjwa wa ovarian cyst. 

 

·     matatizo ya mirija ya uzazi

ovari zimeunganishwa kwenye  mirija ambayo hupitisha mayai kwenda kwenye mfuko wa uzazi ,wakati mwingine mirija hiyo huziba kwa sababu mbalimbali hivyo mayai hushindwa kupita na kusababisha ugumba ,mfano ugonjwa wa endometriosis, upasuaji na peritonitis. 

 

·     matatizo ya kizazi

kizazi ndio sehemu kuu ambayo mtoto hutunzwa na kuishi kwa miezi yote tisa, tatizo lolote linaloshambulia kizazi huleta ugumba, mfano, makovu ndani ya kizazi, uvimbe ndani ya kizazi, kugeuka kwa kizazi na magonjwa ya zinaa kama kaswende na kadhalika. 

 

·     Kansa

 kansa ya kizazi huzuia yai la mama lililorutubishwa kushindwa kujiweka kwenye kizazi ili kukua, hivyo huchangia sana mimba kuharibika au kutotungwa kabisa. 

 

·     matatizo ya mlango wa uzazi

 oparesheni za kizazi, utoaji wa mimba na magonjwa ya zinaa huweza kusababisha kuziba kwa mlango wa uzazi hivyo mbegu za kiume kushindwa kabisa kupita kwenye mlango wa uzazi na kusababisha ugumba. 

 

·     magonjwa mengine ya mwili

 magonjwa yeyote ya binadamu  ambayo huingilia mfumo wa homoni za uzazi huleta ugumba mfano magonjwa ya ini,kisukari, hyperthyrodism, na kadhalika. 

 

·     matumizi ya sigara na pombe

  unywaji wa pombe sana na uvutaji wa bangi huzuia yai kutoka kwenye ovari, lakini pia uvutaji wa sigara hupunguza uwezo wa yai kutembea kutoka kwenye ovari kwenda kwenye mfuko wa uzazi na wakati mwingine husababisha mimba kutunga nje ya kizazi. 

 

·     msongo mkubwa wa mawazo

 ukiwa unatafuta mtoto tayari ukiwa umepaniki kwamba huenda usimpate husababisha inasababisha mwili kutoa homoni kitaalamu kama cortisol ambazo huzuia kazi za homoni za uzazi kitaalamu kama gonadotrophin releasing hormone hivyo hali huzidi kua mbaya. 

 

·     uzito uliopitiliza

 mwili mkubwa unaingilia mfumo wa utengenezaji homoni za uzazi hivyo huweza kuleta ugumba katika umri mdogo sana, hivyo kupunguza uzito ni moja ya njia bora kabisa ya kujiweka kwenye mazingira mazuri ya kuzuia ugumba. 

 

 

·      Maambukizi Ya Wadudu

Maambukizi ya virusi na bacteria yanayoenezwa kwa ngono husababisha makovu na uharibifu, kwa mfano, maambukizi ya Hydrosalpnix yanayosababisha mirija ya uzazi kuziba pande zote na kujaa maji .

 

·      Magonjwa ya Tumbo

Magonjwa ya appendicitis na colitis huleta madhara kwenye tumbo ambayo yanayoweza kuiathiri mirija ya uazazi kwa kujenga makovu au kuiziba.

·      Upasuaji

 

Hii ni sababu kubwa ya magonjwa na uharibifu wa mirija ya uzazi. Upasuaji wa kwenye maeneo ya kinena na tumbo huweza kusababisha uharibifu utakaozuia upitaji wa yai.

 

 

 

·      Matatizo Ya Kuzaliwa Nayo

Mara chache huweza kutokea kuwa mwanamke akazaliwa akiwa na dosari katika mirija yake ya uzazi.

 

 

 


 

 

USHAURI WAKE NINI

Aliwataka wanawake  kabla hawajaanza kuzunguka kwa waganga wa kienyeji na hospitalini ni bora kujichunguza kwa makini  kama wako kwenye hatari zinazoelezewa na kubainisha kuwa  hakuna dawa moja ambayo ina uwezo wa kutibu ugumba kwa watu wote bila kutibu chanzo chake kwanza

 

Alisema  kuwa  kila mtu ana dawa yake ya ugumba kulingana na historia ya maisha yake na chanzo cha tatizo lake, pia wapo wanaoweza kupona kabisa kulingana na chanzo cha tatizo na hali ya ugonjwa ilivyo pia  wapo wasioweza kupona kabisa kama ugonjwa umesha kaa  sana

 




 

Aidha aliwataka wanawake hususani mabinti kuacha baadhi ya tabia   ambazo zimeainishwa  ili kuepuka na tatizo hili la ugumba.

 

Elimu ya madhara ya utoaji mimba katika umri mdogo itolewe ili tatizo hilo liweze kumalizika kabisa .

 habari hii imeandikwa na   mwandishi wa habari Woinde Shizza

 

 

 

 


 

 

 

 

 

 

 

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

إرسال تعليق

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia