WADAU WA UTALII NA UTAMADUNI YATUMIENI MATAMASHA KUKUZA UTALII NCHINI GEKUL


Naibu Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo Pauline Gekul amewataka wadau wa Utamaduni na Utalii nchini kuyatumia kimkakati matamasha ya Utamaduni yanayoendelea nchini kwa lengo la kukuza Utalii.

Gekul ameyasema hayo alipokuwa Mgeni Rasmi wakati akizindua Tamasha la Maasai Festival linalotaraji kufanyika mwezi wa nane mwakani Jijini Arusha ambapo ameipongeza Taasisi hiyo kwa ubunifu na kukuza utalii.

Amesema kwamba wakati huu ni muafaka kwa wadau kuungana na serikali katika kuongeza mazao ya Utalii hapa nchini kwa kuongeza thamani ya shughuli mbalimbali za Utamaduni na Sanaa zenye upekee ikiwemo za Utamaduni wa Kimaasai kwa ajili ya soko la ndani na nje ya nchi.

"Serikali ya awamu ya sita inathamini juhudi za wadau mbalimbali za kutumia shughuli za Utamaduni na Sanaa kwa ajili ya maendeleo ya sekta nyingine ndio maana Rais Samia alielekeza Tarehe 22 January akiwa Moshi serikali na wadau kuyatumia matamasha kimkakati kukuza Utalii"

Awali akitoa Salamu za wizara hiyo Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt.Pindi Chana amesema kwamba Maasai Festival ni bidhaa muhimu ya Utalii katika soko la hapa nchini na waandaaji wamethibitisha hilo kwa vitendo kwamba Utamaduni na Utalii ni kama bidhaa Moja.

Aidha aliwashukuru waandaaji hao wa Maasai Festival kwa kuendelea kukuza na kuimarisha sekta mtambuka kwani Tanzania ni Moja ya mataifa yaliotajwa kuwa na utajiri   wa kipekee katika sekta ya Utamaduni na malikale.

Kwa Upande wake Mkurugenzi wa Wonderland Afrika na View Point Adventures Safaris LTD Said Maulid amesema kwamba zaidi ya wageni 1500 kutoka mataifa ya Ulaya wanatarajiwa kishiriki Tamasha hilo litakaloenda na matukio manne.

Ameyataja Matukio hayo ni pamoja na Warsha,Ukimbiaji wa mbio(Maasai Jogging Bonanza) Onyesho la Mavazi(Maasai Fashion Night) na Maasai Festival CSR yote hayo yatakuwa ni matukio yatayofanyika katika Tamasha la Maasai Festival mwakani mwezi wa nane.

"Natoa wito kwa wadau mbalimbali kuendelea kuunga mkono juhudi za Rais wetu Mpendwa Samia Suluhu Hassan kwani tunaona Royal Tour imejibu hivyo tuanzishe na kujenga ubunifu wa kuanzisha matamasha na bidhaa za Utalii na Utamaduni zitakazosaidia kutangaza nchi yetu kama alivyofanya Rais wetu"

 

About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

إرسال تعليق

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia