KADI YA NJANO SULUHISHO LA JUKWAA LA UBADILISHAJI MALI

 


UJIO wa kadi ya njano tayari ni jukwaa la ubadilishaji wa mali kwa njia ya kidigiti linalokua kwa kasi zaidi na salama barani Afrika

 

Mtu akikata bima ya kadi ya Njano ya mtu wa tatu inaruhusu kuweza kupita na gari katika nchi zilizotuzunguka ikiwemo Zambia Malawi, Zimbabwe, Uganda Rwanda ,Burundi ,Msumbiji ,Jibuti , Sudani kusini na Sudan bila kusimamishwa na iwapo atasababisha madhara yoyote kwa mtu wa tatu bima itagharamia gharama zote za kumlipa

 

 

Naibu  waziri wa fedha ,Hamad Chande amewataka watanzania kutumia fursa ya bima ya kimataifa ya mtu wa tatu (Yellow Card) kama njia moja wapo ya kukuza biashara na uchumi wa nchi na kuwarahisishia wafanyabiashara wanaosafiri kibiashara nje ya nchi.

 

Chande ameyasema hayo wakati akifungua mkutano wa 36 wa baraza la usimamizi wa bima ya mtu wa tatu NIC, unaokutanisha wanachama  wa Soko la pamoja la Mashariki na kusini mwa afrika (COMESA) na wasiowanachama ,unaofanyika  kwa siku tatu jijini Arusha. 

 

Aliwataka wananchi na wafanyabiashara kutumia yellow kadi halisi na sio feki kama ilivyo kwa baadhi ya watu ambao wamekuwa wakihujumu taifa kwa kufumia kadi zisizosahihi.

 

Alifafanua kuwa faida ya yellow kadi unaweza kuitumia popote katika nchi  yoyote wanachama ili kukinga biashara au ajali ukiwa nje ya nchi.

 

"Unapokata  kadi ya Njano Tanzania unaweza kutumia kadi ile ile nchi za jirani kwa thamani ile ile ulionunua katika nchi husika na hii ni faida kubwa kibiashara kwa wafanyabiashara wanaochukua ama kupeleka bidhaa nje ya nchi"alisema

 

Alisisitiza kuwa unapokuwa na kadi ya njano ni kinga kwa biashara hasa pale kunapotokea dharura ya ajali ya gari au ya moto katika biashara kunakufanya usisononoke kwa kuwa bima hiyo itakulipa fidia mali zako.

 

Aliitaka baraza la msimamizi wa bima ya mtu wa tatu (yellow kadi)kulipa fidia kwa waathirika wakati ndani ya simu 30 ili mtu awe na imani na mashirika ya bima.

 

Awali mkurugenzi mtendaji shirika la bima nchini NIC dkt Rehema Dorie alisema kuwa mkutano huo unakutanisha nchi wanachama wa soko la pamoja la mashariki na kusini mwa afrika (COMESA) na wasio wanachama zinazofanyabiashara ya bima ya mtu wa tatu.

 

Dkt Dolie ambaye pia ni mwenyekiti wa baraza la usimamizi wa bima ya mtu wa tatu kwa nchi za COMESA alisema yellow kadi inampa kinga na kumrahisishia mfanyabiashara anayesafiri ama kusafirisha mizigo katika nchi za comesa  bila hofu ukizingatia kwamba Tanzania ni kitovu cha biashara kwa kuwa inabandari kubwa zinazopokea mizigo .

 

" hii inalipa mara moja kutokana na sheria za nchi husika bila kujali gharama zilizopo".

 

Dkt Dolie ambaye pia ni mwenyekiti wa baraza la usimamizi wa bima ya mtu wa tatu kwa nchi za COMESA alisema yellow kadi inampa kinga na kumrahisishia mfanyabiashara anayesafiri ama kusafirisha mizigo katika nchi za comesa  bila hofu


habari hii imeandikwa na mwandishi Woinde Shizza,Arusha 


About Woinde Shizza

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

إرسال تعليق

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia