Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Sara Kibwana
amesema Halmashauri ya Wilaya ya Meru imeibuka mshindi wa kwanza na wa
jumla ngazi ya Mkoa kwenye mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma
Shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA) yaliyofanyika tarehe 06 Juni 2018
hadi 10 Juni 2018 ambapo Halmashauri 7 za Mkoa wa Arusha zilishiriki .
Kibwana alisema siri ya ushindi huo ni pamoja na maandalizi
mazuri yaliyofanyika kwani Halmashauri hiyo ilitoa maelekezo zaidi ya
miezi 9 iliyopita kwa Walimu Wakuu wa Shule za Msingi kuhakikisha kila
wiki wanafunzi wanakua nasiku za kufanya michezo pia maandalizi
yalikuwa mazuri wakati wa michezo kwakuwa wachezaji walijiandaa
kikamilifu kwa kukaa siku 5 kambini.
Naye Afisa utamaduni wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru, Senyaeli
Pallangyo alisema uchaguzi wa wachezaji kwa kuzingatia viwango
uliofanyika kuanzia ngazi ya chini hadi Wilaya umechangia ushindi huo
mkubwa ikiwa ni pamoja na uwezo wa makocha sambamba na wachezaji kuwa
na nidhamu ya hali ya juu na kufuata taratibu za michezo .
Jumla ya wachezaji 25 kutoka timu mbalimbali za Halmashauri yaWilaya
ya Meru na Makocha 4 wamechaguliwa kuunda timu ya Mkoa wa Arusha .
Ikumbukwe kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Meru kwa mwaka huu 2018
imekuwa mshindi wa kwanza na wajumla kwa ngazi ya Mkoa wa Arusha wenye
Halmashauri 7 katika mashindano ya michezo ya umoja wa michezo Shule za
Sekondari Tanzania ( UMISSETA) na umoja wa michezo na taaluma shule za
Msingi Tanzania (UMITASHUMTA) na kuzawadiwa jumla ya Makombe ya ushindi
10