Na Woinde Shizza,Arusha
Shule ya Sekondari Kisimiri iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Meru
,Mkoani Arusha imefanya vizuri kwenye matokeo ya kidato cha sita kwa
kushika nafasi ya pili kitaifa kati ya shule 543 zilizofanya mtihani
huo, huku shule ya Sekondari Kibaha ikishika nafasi ya kwanza na shule
ya Sekondari Kemebos ikishika nafasi ya tatu,hii ni kwa mujibu wa
matokeo yaliyotangazwa na baraza la mitihani Taifa.
Aidha matokeo haya ya shule ya Sekondari Kisimiri ni mwendelezo wa
historia ya kufanya vizuri katika matokeo ya mitihani hiyo ya kidato cha
sita kwani kwa miaka 3 mfululizo imekuwa kwenye kundi la shule tatu
bora kitaifa ,ambapo mwaka 2016 ilishika nafasi ya kwanza,mwaka 2017
ikashika nafasi ya tatu na kwa mwaka huu 2018 imeshika nafasi ya pili
kitaifa kwa watahiniwa wake 67 kupata daraja la kwanza na la pili ikiwa
51 kati yao wamepata daraja la kwanza na 16 kupata daraja la pili.
Nuru ya shule hii ya Sekondari Kisimiri yazidi kuangaza kwenye Mkoa
wa Arusha wenye shule 31 zenye watahiniwa zaidi ya 30 za Serikali na
Binafsi kwani ni shule pekee ya Serikali kushika nafasi ya kwanza mkoani
hapa kwa kipindi cha miaka 3 mfululizo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Ndg. Christopher
Kazeri alipokuwa akiwapongeza walimu wa Shule ya Sekondari Kisimiri kwa
jitihada zao zilizo ifanya shule hiyo kuwa mshindi wa pili kitaifa
katika matokeo ya kidato cha sita kwa mwaka huu 2018, pia amewasihi
walimu hao kuongeza bidii katika ufundishaji ili kupata matokeo mazuri
zaidi kwa kushika nafasi ya kwanza Kitaifa.
Mkurugenzi huyo ametoa pongezi hizo alipotembelea Shule hiyo kwa
Lengo la Kuwapongeza Walimu pamoja na kusikiliza na kutatuo changamoto
wanazokabiliana nazo ili kuleta tija zaidi kwenye taaluma ya Shule hiyo.
Makamu mkuu wa shule ya Sekondari Kisimiri Mwl. John Awe amesema kuwa
mojawapo ya mbinu zilizotumika kuhakikisha shule hiyo inapata matokeo
mazuri illikuwa kutoa mafunzo ya ziada kwa wanafunzi ambao walikuwa na
uwezo mdogo, hivyo walimu walitenga muda wa ziada kuwafundisha wanafunzi
hao ambao wengi wao walifanya vibaya kwenye mtihani wa utamirifu (MOCK)
kwa kupata alama sifuri.Ameongeza pia walimu wana moyo wa kufundisha
kwa kutoa mfano kuwa kwenda darasani ni swala moja na kufundisha kama
inavyotakiwa na wanafunzi kuelewa ni jambo jingine .
Nao Walimu wametoa changamoto zinazoikabili Shule hiyo ni upungufu wa
viti vya walimu 50 pamoja na madawati ya wanafunzi 300 pia walimu hao
wamehitaji ufafanuzi wa maslai yao kama watumishi ikiwemo kupanda
daraja,
Akitoa ufafanuzi wa maswala ya watumishi Mkuu wa Idara ya Utawala na
Rasilimali watu .Grace Mbilinyi ameeleza kuwa kutokana na zoezi la
kuwabaini watumishi hewa na wenye vyeti vya kugushi Serikali ilisitasha
upandaji madara kwa watumishi wa umma ila kwa sasa maelekezo mbalimbali
yanatolewa ambapo zoezi hilo linaendelea kwa awamu pia
Kuhusu swala la malipo ya likizo amewasihi walimu kuwa makini kwa
kuweka viambatanisho vyote muhimu vikiwemo vyeti vya watoto vya kuzaliwa
na vyeti vya ndoa pia ametoa angalizo la udanganyifu kwa kugushi vyeti
hivyo.