Ticker

6/recent/ticker-posts

Kheri James Azindua kampeni kwa kishindo Arusha kata zote 77 kuchukuliwa na ccm




Mwenyekiti wa Uvccm Taifa na MCC Ndg. Kheri James Leo amezindua kampeni katika kata ya Daraja Mbili Mkoani Arusha ambapo amesema chama cha Mapinduzi kitashinda kata zote 77 nchini zinazofanya uchaguzi wa marudio.

Akimnadi mgombea wa kata hiyo kwa tiketi ya Ccm Ndg. Prosper Msofe Ndg. kheri james amesema ushindi huu unatokana na muamko wa wananchi juu ya utendaji na kasi ya Rais  John Pombe Magufuli dhidi ya kutatua kero  na matatizo yanayowakabili wananchi.

Miongoni mwa  kero mbalimbali zilizotatuliwa kwa kipindi kifupi ni maji,miundombinu ya barabara  Elimu bure na sasa serikali inaendelea kutatua changamoto ya umeme katika mradi wa Rea  awamu ya tatu sambamba na treni ya umeme.

Akimnadi mgombea huyo amewataka wananchi wa eneo hilo  kumchagua diwani wa kata hiyo kwa kuwa ni Mtendaji na alikuwa akikwamishwa wakati akiwa upinzani kutoka na na chama alichokuwepo kupinga ilani ya CCM.

Ameongeza kuwa kwa sasa itakuwa rahisi kwa yeye kutetea shida za wananchi kutoka na na hakuna wa kumkwamisha.

Kwa upande wake mgombea udiwani Prosper Msofe ameahidi kuendeleza Yale mazuri aliyekuwa akijaribu kuyafanya awali ikiwemo kuhakikisha kina mama na Vijana wanapata mikopo, kero ya ukosefu wa ofisi katika baadhi ya Shule inatatuliwa, Pamoja na uboreshaji wa miundombinu ya Barabara katika kata hiyo.

Matukio mbalimbali katika picha.















Post a Comment

0 Comments