Ticker

6/recent/ticker-posts

RAIS SAMIA MGENI RASMI MEI MOSI KITAIFA ARUSHA,TUCTA YACHACHAMAA ATAKA MISHAHARA KWA WAFANYAKAZI IWE JU




RAIS Samia suluhu Hasani anatarajiwa kuwa mgeni Rasmi katika maadhimisho ya sikukuu ya wafanyakazi duniani ,Mei Mosi yanayotarajiwa kufanyika kitaifa Mkoani Arusha.

Akiongea na vyombo vya habari Mkoani hapa, Rais wa Shirikisho la wafanyakazi Tanzania,TUCTA, Tumaini Nyamhokya alisema maadhimisho hayo yatafanyika katika uwanja wa mpira wa Sheikhe Amri Abeid siku ya Mei Mosi.

Alisema kauli mbiu ya mwaka huu inayosema,"Nyongeza ya Mishahara ni Msingi wa Mafao Bora na Kinga dhidi ya Hali Ngumu ya Maisha" inaakisi uhalisia wa Maisha ya wafanyakazi kwa sasa kwani gharama za maisha zimepanda na mishahara haikidhi Mahitaji ya kila siku ya Mfanyakazi.


Alisema mishahara ikiwa bora itawezesha mafao kuwa bora pia wakati wa kushtaafu .

"Hivyo basi tumeona ni Vema kutumia siku yetu hii muhimu ya Sherehe za Wafanyakazi kuikumbusha serikali na waajiri wote umuhimu wa kuwa na Mishahara bora inayoendana na hali halisi ya maisha tukiwa Kazini na baada ya kustaafu"

Post a Comment

0 Comments