Judith Ferdinand, Mwanza
Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) limehimizwa
kuwa makini na kufanya maamuzi sahihi katika michezo iliyosalia katika
ligi daraja la kwanza ili kuhakikisha timu itakayopanda ligi kuu ni
iliyo na sifa.
Hayo yamesemwa na kocha mkuu wa timu ya Alliance Sports
Club ya Jijini Mwanza, Mbwana Makata alipokuwa akizungumza BMG wakati
mazoezi katika uwanja mkongwe wa Nyamagana.
“Sisi Alliance tunaimani timu yetu ni bora na itafikia
mafanikio,hivyo tunaomba TFF na Bodi ya Ligi, katika michezo hii ya
mwisho,waweze kuwa makini na maamuzi pamoja na waamuzi wachezeshe
michezo kwa kufuata sheria na kanuni za mpira, ili kuhakikisha timu
inayopanda ligi kuu ni yenye sifa,”alisema Makata.
Pia alisema timu hiyo inaongoza kwenye kundi lao la C kwa
pointi 19,ikifatiwa na Dodoma FC 18 na Biashara ya Musoma ikiwa na
pointi 17,hivyo ushindani katika kindi hilo ni mkubwa kwani timu zote
zinahitaji ushindi na anaimani timu yao ni bora, itaweza kufikia
mafanikio sambamba na kufanya vizuri.
Hata hivyo,aliwaomba mashabiki kushabikia timu hiyo katika
mechi zao ziliosalia ambapo mchezo unafuatia watakutana na Dodoma FC
katika uwanja wa Mpwapwa mkoani Dodoma desemba mwishoni,sambamba na
kutoa sapoti ili kuweza kuwapa hamasa na nguvu na hatimaye kufanya
vizuri.
Kwa upande wake Nahodha wa Alliance Hance Masoud alisema
wanafuata maelekezo kutoka kwa walimu wao, ili kufanya vizuri na
kujipanga vyema katika mchezo wao na Dodoma FC na mingine iliyosalia.
Masoud alisema,ni kweli kundi C ni gumu na kila mtu anatoa
macho kwa sababu anahitaji ushindi na hatimaye kufuzu kuingia ligi kuu,
kwani kujiandaa na kujipanga vyema husaidia kufanya vema kwenye mechi.
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia