Ticker

6/recent/ticker-posts

WAFANYA BIASHARA WADOGO SOKO LA TENGERU WAKUBALI KUTOKA BARABARA



Na Woinde Shizza,Arusha
wafanya biashara wa soko la Tengeru lililopo ndani ya  Halmashauri ya Wilaya ya Meru  wameunga mkono  zoezi la kuwaondoa wafanya biashara  wa mazao  barabarani kwa kuwaingiza katika eneo la soko.
Afisa biashara ambaye ni msimamizi wa masoko Elibariki Nnko ameeleza kuwa  zoezi hilo limeanza rasmi baada ya baadhi ya wafanya biashara kukaidi kutumia eneo la soko lililojengwa  kwa gharama kubwa na kuendelea kupanga bidhaa zao barabarani ikiwa ni kuatarisha maisha yao.

 Aidha alifafanua kuwa  Halmashauri hiyo inaendelea na uboreshaji wa  miundombinu  kwenye soko hilo kwani mpaka  sasa   kiasi cha sh. milioni 20 zimetengwa kwa ajili ya kutengeneza meza za sokoni hapo .
Elisifa Boniface ambaye ni mfanyabiashara kwenye soko hilo alisema kuwa  wateja wengi hawaingii ndani ya soko kwani hupata mahitaji yao nje ya soko jambo linalo athiri biashara yake na wafanya biashara wenzake waliopo ndani ya soko.
kwa upande wake  Mary Pallangyo ambaye ni mfanya biashara wa mbogamboga ameiomba Halmashauri hiyo kuboresha miundombinu  ikiwa ni pamoja na kukamilisha uwekaji paa kwenye baadhi ya maeneo ya soko hilo.
pia kuna  baadhi ya wafanya biashara walio kuwa wakipanga bidhaa zao barabarani wameiomba Serikali kuwaruhusu kuendelea kujitafutia risiki kwa njia hiyo.

Post a Comment

0 Comments