MAKONDA ATEMBELEA KAMBI YA MATIBABU KALOLENI, ATOA WITO HUDUMA KUTOLEWA BILA UBAGUZI
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Mbunge wa Arusha Mjini, Mhe. Paul Christian Makonda, ametembelea wananchi wanaopata huduma katika kambi ya matibabu inayofanyika Hospitali ya Wilaya ya Kaloleni jijini Arusha, ambapo alipata fursa ya kuzungumza na wagonjwa pamoja na kujionea huduma zinazotolewa na wataalamu wa afya.
Katika ziara hiyo, Makonda aliwapongeza madaktari, wauguzi na watumishi wa afya kwa juhudi zao za kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora kwa wakati. Aidha, amesisitiza kuwa kila mwananchi anayefika katika kambi hiyo anapaswa kupatiwa huduma stahiki bila ubaguzi wowote.
“Hakikisheni hakuna mwananchi anayerejea nyumbani bila kupata matibabu anayostahili,” amesema Makonda.
Pia ameeleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuimarisha sekta ya afya kwa kusogeza huduma karibu na wananchi ili kuongeza upatikanaji wa huduma bora na za kisasa.
Kwa upande wao, wananchi waliojitokeza katika kambi hiyo wamepongeza huduma zinazotolewa pamoja na ujio wa Waziri Makonda ambao umeongeza faraja na matumaini kwa wagonjwa waliokuwa wakipatiwa matibabu.
#AfyaKwaWote #Arusha #Kaloleni #Tanzania #SamiaSuluhuHassan


























0 Comments:
Post a Comment
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia