Afisa mifugo
ya meru Dr. Amani Sanga akizungumza katika kilele cha maadhimisho ya siku ya Mazingira duniani na wananchi wa kijiji cha Ngyani kilichopo katika kata ya
Nkwaranga ndani ya halmashauri ya meru niaba ya mgeni ramsi ambaye mkuu wa
wilaya ya meru
Afisa Maendeleo ya Jamii wa bonde la pangani Abraham Yesaya akiwa anaelezea shughuli ambazo wanazifanya wao kama bonge la pangani |
Woinde Shizza, Arusha
WAKATI
Mataifa mbalimbali yanaadhimisha Siku ya Mazingira Duniani iliofikia
kilele chake hapo Jana Juni 5, 2018, halmashauri ya wilaya ya Meru
imeathimisha kwa kupanda miti 7000 huku miti 500ikiwaimepandwa katika
siku ya kilele chamaathimisho haya Pamoja na kuweka bikoni katika mipaka
inayozunguka vyanzo vya maji vilivyopo ndani ya halmashauri hiyo.
Kwa
miaka mingi siku ya Mazingira duniani imekuwa ikiadhimishwa kwa Wadau
katika nchi mbalimbali kuchukua hatua chanya zinazohusu mazingira. Siku
hii pia imekuwa ni sehemu ya kampeni ya utoaji elimu juu ya maswala
yanayojitokeza kuhusiana na mazingira.
Kauli
mbiu katika maadhimisho ya mwaka huu inasema “MKAA NI GARAMA TUMIA
NISHATI MBADALA” ikihamasisha jamii kuwa na urafiki endelevu na
mazingira asilia ambapo kila mtu anapaswa kutambua, kufurahi, kujivunia
na kulinda uzuri wa mazingira asilia na kuhamasishana ili kuyatunza na
kuyahifadhi.
Akizungumza
katika kilele cha maadhimisho ya siku ya Mazingira duniani Afisa mifugo
ya meru Dr. Amani Sanga Kwanza niaba ya mgeni ramsi ambaye mkuu wa
wilaya ya meru alisema Kuwa Tanzania kama ilivyo kwa nchi nyingi Barani
Afrika na duniani kwa ujumla imeendelea kuathirika kwa kiasi kikubwa na
uharibifu wa mazingira unaotokana na shughuli mbalimbali zikiwemo za
kilimo, ufugaji, ujenzi n.k
Uharibifu
huu wa misitu hutokana na shughuli za kilimo na ufugaji kwa njia zisizo
endelevu. Uharibifu huu wa misitu unachangia pia kukosekana kwa mvua,
kukauka kwa mito, mabwawa na uoto wa asili.
Aisha
alibainisha kuwa kazi ya kuhamasisha na kuelimisha jamii kuhusu umuhimu
wa kuhifadhi mazingira inahitaji ushirikiano wa Wadau katika ngazi
zote.
Alisema
halmashauri ya Meru katika kuazimisha siku hii imepata ushirikiano
kutoka Kwa wadau mbalimbali wakiwemo bonde la pangani, mali hai
klabu,kili flora, mamlaka ya making mjimdogo wa usa river Pamoja na
SUAMA.
Taasisi na Asasi za Kiraia zikishirikiana katika kutekeleza kikamilifu
Sheria na Kanuni za uhifadhi wa mazingira nchini ili in a inasaidia
kupunguza kwa kiasi kikubwa uharibifu wa mazingira.
Kwa
upande wake Afisa Maendeleo ya Jamii wa bonde la pangani Abraham
Yesaya alisema Kuwa Katika kilele cha maadhimisho haya Wametoa jumla ya
miti 7000 ambayo imepandwa katika Kata 12 na kutoa elimu ya misitu
katika shule zaidi ya 20.
Alisema
ni wajibu wa mamlaka katika ngazi mbalimbali ziwe na Mipango bora ya
ardhi, mikakati ya uhifadhi wa vyanzo vya maji, pamoja na udhibiti wa
uvunaji holela wa misitu na ufugaji usio endelevu Pamoja na kutoa elimu
juu umuhimu wa kutunza mazingira na faida zinazopatikana ili Wananchi
waunge mkono jitihada zinazofanywa katika kulinda na kuhifandhi
mazingira kwa faida ya kizazi cha sasa na kijacho.
“Usafi
wa mazingira uhusishe kila mtu kuhakikisha taka haswa Za plastiki
zinakusanywa na zinatupwa katika maeneo yaliyotengwa na tupande miti
mingi wakati wa msimu wa mvua ili tujihami na kuenea kwa hali ya jangwa
na mabadiliko ya tabianchi” alisema Yesaya
Alisema,
maliasili zilizopo zinahitajika kwa matumizi ya vizazi vilivyopo na
vijavyo, hivyo uwepo wake hutegemea zaidi uhifadhi wa rasilimali hizo
na matumizi katika jamii iliopo na ijayo.
kwa
upande wake mwenyekiti wa kijiji cha Ngyani kilichopo katika kata ya
Nkwaranga katika halmashauri ya meru Elishilia Mathayo alisema
anashukuru sana halmashauri ya meru kwakuwaekia mipaka na bikoni katika
kwenye maeneo ya vyanzo vya maji kwani hii itasaidia kuonyesha wananchi
wanaofanya shughuli za kibinadamu Kujua mipaka yao ya kufanya shughuli
hizo na hii itasaidia kuendelea kutunza vyanzo vyetu vya maji
Alisema
Kama ilivyo Madhumuni ya maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ni
kuhamasisha jamii kuelewa masuala yahusuyo mazingira na kuchukua hatua
za kuhifadhi na kulinda mazingira na kama Kauli Mbiu iliyoongoza
maadhimisho haya kimataifa ni “tokomeza uchafuzi wa plasicki”, huku
kitaifa Kauli mbiu ikiwa inasema "mkaa gharama tumia nishati mbadala."
lengo likiwa ni kuhamasisha utunzaji wa mazingira hivyo niwajibu wa kila mtu kutunza mazingira na mazingira yamtunze.
mgeni rasmi akipanda moja ya miti
baadhi ya wadau wa SUAMA wakisikiliza hutuba ya mgeni rasmi mara baada ya kufanya zoezi la uhoteshaji miti
mwenyekiti wa kijiji cha Ngyani kilichopo katika kata ya
Nkwaranga katika halmashauri ya meru Elishilia Mathayo akizungumza katika maadhimisho hayo
mmoja wa wananchi ambaye jina lake halikufahamika akitoa dukuduku lake mbele ya mgeni rasmi ambapo aliomba zoezi hili la upandaji miti liwe endelevu
mbali na upandaji miti pamoja na uelimishaji juu ya utunzaji wa mazingira pia halmashauri ya meru kwa kushirikiana na bonde la pangani waliandaa maonyesho ya majiko mbalimbali ambayo yanatunza mazingira kama kauli mbiu inavyosema mkaa ni gharama tumia nishati mbadala