Na
Woinde Shizza ,Arusha.
Wilaya ya
Karatu imegawa maeneo kwa Wafanyabiashara wadogo wadogo maarufu kama Mama
Ntilie na Wamachinga ili kuepusha migogoro ya mara kwa mara inayojitokeza
kufuatia Wafanyabiashara hao kufanya shughuli zao maeoneo yasiyo rasmi na
kujikuta wakifukuzwa .
Mkuu wa
Wilaya hiyo Bi.Theresia Mahongo amesema kuwa Wilaya hiyo imeamua kuwatengea
maeoneo katika eneo la Mnadani ili kumaliza mgogoro uliokuwepo tangu mwaka 2000
baada ya Wafanyabiashara hao waliokua wakifanya biashara pembezoni mwa barabara
kuondolewa ili kupisha ujenzi wa barabara ya Karatu /geti la Ngorongoro.
Bi.Theresia
amesema kuwa wamewagawia maeoneo hayo ambayo wanaweza kujenga vibanda na kuweka
mkataba na halmashauri juu ya ulipaji wa kodi ili waweze kufanya kazi zao bila
kubughudhiwa na kujipatia kipato cha kila siku
Alisema kuwa
jumla ya Wafanyabiashara 34 watagaiwa maeneo katika eneo la mnadani ambapo
wanatarajia kulitumia eneo hilo katika biashara ndogo ndogo kwani wanatarajia
kuwa eneo hilo litaendelezwa na kuwa na mzunguko mkubwa wa biashara.
Mkurugenzi
wa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Waziri Mourice amesema kuwa wataandaa
mikataba ambayo itawasilisha maslahi ya pande zote mbili ,na kuongeza kuwa
mpango huo unalenga kuwawezesha wananchi wanyonge kupata maeneo ya kufanya
shughuli zao kama ilivyo serikali ya awamu ya tano ambayo imejipambanua
kuwahudumia wananchi wanyonge.
“,Mpaka
tarehe 15 mwezi huu tutakua tumeandaa
mikataba baina ya halmashauri na wafanyabiashara ili waweze kuwa huru kujenga
vibanda vyao na kuanza ujenzi na kufanya
shughuli zao” Alisema Mkurugenzi
Kwa Upande
wao Wafanyabiashara hao Evelina Hando na
Fausta Saria wameishukuru
serikali kwa kusikiliza kilio chao cha muda mrefu cha kuwapatia maeoneo ya
kufanya shughuli zao kwani kwa muda mrefu walikua wakiteseka na kukosa maeoneo
rasmi.
Evelina alisema
kuwa wamekua wakiteseka tangu mwaka 2000
wamehamishwa mara kwa mara na kuibuka migogoro kati yao na wamiliki wa
maeneo walipokuwa wanafanyia biashara lakini kwa sasa wanaishukuru serikali kwa kuwapatia maeneo hayo.