Ticker

6/recent/ticker-posts

UJENZI NA UBORESHAJI WA KITUO CHA AFYA USA-RIVER NI MFANO WA KUIGWA.


 
Naibu waziri Ofisi ya Raisi TAMISEMI Mhe. Josephat Kandege ameridhishwa na matumizi ya fedha kwenye ujenzi na uboreshaji wa Kituo cha Afya Usa- River  na kueleza kuwa  thamani ya fedha imeonekana pia ametoa  wito kwa Halmashauri nyingine kuiga mfano.
Mhe.Naibu Waziri Kandege amesema hayo alipokagua ujenzi na ukarabati wa kituo cha Afya Usa- River wakati wa ziara ya kukagua ujenzi wa vituo vya Afya vilivyopewa fedha na Serikali kwenye Mkoa wa Arusha kwaajili ya ujenzi wa majengo mapya na kukarabati yaliyopo kwa lengo la kutoa huduma bora za Afya,  pia Mhe.Naibu Waziri Kandege amemwagiza Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Dkt. Cosmas Kilasara kutoa elimu ya kina kwa wananchi ili waweze kujiunga na mfuko wa Afya ya jamii CHF.
Aidha ujenzi wa miundombinu mbalimbali kwenye  kituo hicho cha Afya Usa -River  ni baada ya Serikali kutoa fedha kiasi cha Sh. milioni 500 kwa ajili ya kuboresha kituo hicho kwa kujenga majengo  mapya ambayo ni jengo la maabara,nyumba ya mtumishi, jengo la upasuaji, wodi ya mama na mtoto, chumba cha kuifadhia maiti, kichomea taka  pamoja na kufanya ukarabati wa majengo yaliyokuwepo kwa lengo la kuwapa wananchi huduma bora za afya na kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi. 


Naibu waziri Ofisi ya Raisi TAMISEM mhe. Josephat Kandege(wakwanza kulia) akiwa na viongozi mbalimbali akiwemo  Katibu Tawala wa Wilaya ya Arumeru, Ndg.Timotheo Mzava,Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Ndg.Christopher Kazeri,Mganga mkuu wa Mkoa wa Arusha Dkt. Timoth Wonanji ,Mganga mkuu wa Halmashauri ya Meru Dkt. Cosmas Kilasara pamoja na wataalamu wenginewakitembelea na kukagua ujenzi kwenye kituo cha Afya Usa-River.
Naibu waziri Ofisi ya Raisi TAMISEM mhe. Josephat Kandege alipotembelea jengo la Upasuaji kwenye kituo cha Afya Usa-River.
Naibu waziri Ofisi ya Raisi TAMISEM mhe. Josephat Kandege alipotembelea jengo la Upasuaji kwenye kituo cha Afya Usa-River.
Naibu waziri Ofisi ya Raisi TAMISEM mhe. Josephat Kandege alipotembelea jengo la kuwahudumia wagonjwa wa wa nje (OPD)
Naibu waziri Ofisi ya Raisi TAMISEM mhe. Josephat Kandege alipotembelea jengo la kuwahudumia wagonjwa wa wa nje (OPD)
Naibu waziri Ofisi ya Raisi TAMISEM mhe. Josephat Kandege alipotembelea jengo la wodi ya mama na mtoto kwenye kituo cha Afya Usa-River.
Naibu waziri Ofisi ya Raisi TAMISEM mhe. Josephat Kandege alipotembelea sehemu ya kufulia iliyopo kwenye wodi ya mama na mtoto kwenye kituo cha Afya Usa-River.
Naibu waziri Ofisi ya Raisi TAMISEM mhe. Josephat Kandege alipotembelea kichomea taka katika Kituo cha Afya Usa-River.
Naibu waziri Ofisi ya Raisi TAMISEM mhe. Josephat Kandege akikagua  upauzi wa njia ya kuptia wagonjwa  .
Naibu waziri Ofisi ya Raisi TAMISEM mhe. Josephat Kandege akitoa mrejesho wa ukaguzi wa  kituo cha Afya Usa-River.
Naibu waziri Ofisi ya Raisi TAMISEM mhe. Josephat Kandege akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Christopher Kazeri .

Post a Comment

0 Comments