Ticker

6/recent/ticker-posts

BAADHI YA VIGOGO WAHAHA VIWANJA VYA WAZI JIJI LA ARUSHA NGOMA MOTO

DSCF0807Mwenyekiti wa kamati hiyo Dk.Khamis Kigwangalla katikati  na Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema  wakipata maelezo kutoka kwa injinia wa jengo la hospitali ya Levolosi hivi karibuni
DSCF0819
DSCF0818
DSCF0817Kamati ikiwa makini kufuatilia mchakato
DSCF0814
Meza kuu ndani ya kikao cha kamati
DSCF0808Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema akiangalia nyufa katika jengo la hospitali ya Levolosi akiwa na Mbunge wa Dole Zanzibar Sylvester Mabumba


Kamati ya Bunge ya serikali za mitaa (TAMISEMI)inaiagiza serikali kuwasimamisha kazi watumishi wote waliohusika katika ugawaji wa viwanja( 20) vyenye mgogoro katika halmashauri ya jiji la Arusha ili kupisha uchunguzi  baada ya kubaini uwepo wa ugawaji usio halali wa viwanja katika maeneo ya wazi katika kipindi cha mwaka 2000 na 2006.
Kauli hiyo ilitolewa hivi karibuni jijini hapa na mwenyekiti wa kamati hiyo Dk.Khamis Kigwangalla wakati akitoa maazimio ya kamati baada ya ziara yao ya siku  nne iliyolenga kukagua miradi mbalimbali na maeneo yenye mgogoro katika Halmashauri ya jiji la Arusha
Aidha katika mkutano huo Mwenyekiti wa kamati hiyo alifanya mahojiano ya kina na wahusika mbele ya kamati na kujiridhisha kuwa kulifanyika ufisadi wa kutisha katika ugawaji wa viwanja hivyo.
Dk.Kigwangalla alisema kuwa kamati hiyo inaiagiza serikali kuwachukulia hatua kali za kisheria kwa watumishi wote waliohusika katika sakata hilo la ugawaji wa viwanja,ikiwepo kuwasimamisha kazi ili kupisha uchunguzi wa kina wa kamati pamoja na kuwapa maelekezo ya namna ya kuripoti kila siku katika eneo husika
Katika ziara hiyo kamati iligundua kuwa nyaraka mbalimbali zinazohusiana na maeneo hayo kuwa na mapungufu makubwa huku ikipelekea viwanja hivyo kugawiwa kinyemela kwa wamiliki wa viwanja hivyo.
Pia kamati hiyo iliazimia kusimamisha vibali vyote vya ujenzi katika maeneo yenye  mgogoro  huku Mwenyekiti wa kamati hiyo akitaja maeneo hayo kuwa ni pamoja na uwanja wa ngarenaro,hospitali ya levolosi,Viwanja vya dampo,na vingine vyenye mgogoro
.Dk Kigwangalla wataja wafanyakazi hao kuwa ni pamoja na aliyekuwa mkuu wa Idara ya Ardhi, Mrimba Maghembe na wa Mipango Miji, Richard Ndagamasa na msaidizi wake, Elly Kirenga, pamoja na mtumishi mwingine aliyemtaja kwa jina moja la Urassa.
Pia katika hali isiyokuwa ya kawaida, Kamati hiyo imeiagiza serikali kuhakikisha inawatafuta, Sadic Abdallah Sadic, anayedaiwa kuuziwa viwanja vingi vyenye mgogoro huku nyaraka zilizo na picha na saini yake zikiwa na walakini na kutakiwa kufikishwa mbele ya kamati hiyo kutokana na kuitwa kwa siku tatu na kushindwa kufika.
Akiongelea kiwanja cha Njiro, alisema kuwa kilitengwa kwa ajili ya ujenzi ya hospitali, kituo cha polisi na mahakama ya tarafa, ambapo ekari nne zilikuwa kwa ajili ya kumfidia mwananchi ambaye eneo lake liliuzwa kwa mtu mwingine.
Alisema kuwa wakati halmashauri ikiwa kwenye mchakato wa kumnyang’anya mwekezaji huyo eneo hilo likauzwa kinyemela kwa mfanyabiashara Cicram Jeetu Patel pamoja na mkewe Sabira, ambao sasa wamebadili jina wanajiita Kampuni ya Njiro Medical Comple.
Hata hivyo Kigwangala alimuomba Rais Jakaya Kikwete kutumia mamlaka yake kisheria kubatilisha hati za ardhi kitalu E Njiro chenye viwanja namba 471 1-20 na kilichokuwa kiwanja cha wazi eneo la Kilombero ambacho kiliuzwa kwa ufisadi kwa ushirikiano baina ya watendaji na waliokuwa madiwani wa CCM, Musa Mkangaa na Mary Kisaka.
Na Pamela Mollel, wa JAMII BLOG
 

Post a Comment

0 Comments