Ticker

6/recent/ticker-posts

DCEA YATEKETEZA ZAIDI YA MAGUNIA 150 UA BANGI NA KUFUNGUA ZAIDI YA KESI 30 ZA KATIKA KAMPENI YAO YA KUDHIBITI DAWA HIZO



Ofisa ustawi ya jamii kutoka mamlaka ya dhitibiti na kupambana na dawa za kulevya Kanda ya kaskazini (DCEA)Sara Ndaba   wa tatu kushoto akiongea na wananchi waliotembelea katika Banda lao lililopo  katika maonyesho ya 30 ya nane nane yanayofanyika njiro  ndani ya jiji la Arusha 

 Na Woinde Shizza , ARUSHA 

 Katika kuhakikisha  matumizi  ya madawa ya kulevya yanaisha kabisa kama sio  yanapungua mamlaka  ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya Kanda ya kaskazini wameteketeza jumla ya magunia 173 ya bangi na kuna  kesi 36 zimefunguliwa .

Hayo yamebainishwa na ofisa ustawi ya jamii kutoka mamlaka ya dhitibiti na kupambana na dawa za kulevya Kanda ya kaskazini (DCEA)Sara Ndaba wakati akiongea na waandishi wa habari katika maonyesho ya 30 ya nane nane yanayofanyika njiro  ndani ya jiji la Arusha ambayo  kauli mbiu yake inasema chagua viongozi bora wa serikali za mitaa Kwa maendeleo  endelevu ya kilimo mifugo na uvuvi.


Aidha aliwataka wakulima ambao wanalima vilimo vya madawa ya kulevya aina ya bangi na mirungi kuacha mara moja kwani ni haramu na kunasheria imeundwa Kwa ajili ya  kuwakamata wale wote ambao wanalima na hatua kali zinachukuliwa dhidi yao.

"Katika maonyesho haya  tumekuwa tukitoa elimu juu ya adhari za  matumizi ya bangi au kilimo cha bangi na pale ambapo mkulima anaweza kuingia vishawishi vya kupata fedha za haraka haraka na kuingia katika Kilimo hicho tunampa elimu asiweze kuingia katika Kilimo hicho maana ni kinyume na Sheria na pale atakapo bainika ataingia kwenye mikono ya Sheria" alisema Sara



Aliwataka wakulima hao  ambao wanalima mazao ya madawa ya kulevya waache badala yake walime mazao ya chakula  ,mazao  ambavyo yanaruhusiwa   ambavyo ni yabiashara lakini wasijiingize katika Kilimo Cha bangi au mirungi.

Alisema hadi Sasa wametoa elimu hiyo Kwa wananchi wa vijiji vya  kisimiri pamoja na losinoni vilivyopo wilaya ya Arumeru maeneo  ambayo yanaongozwa kwa kulima bangi na wamewataka wakulima hao kulima  mazao mengine   na kuachana na bangi na mirungi .

Alibainisha kuwa wakulima hao walieleza sababu ya kulima mazao hayo kuwa ni ukosefu wa maji pamoja na miundo mbinu ya barabara  ambapo alisema baada ya kutoa elimu walienda kufanya tasmini  wakiwa na ma ofisa kutoka ofisi ya mkuu wa mkoa na kwenda kuwaeleza namna gani  watachanganua matatizo hayo yakiwemo ya barabara pamoja na maji


 Aidha alibainisha kuwa katika kuendeleza  kutoa elimu  mkuu wa wilaya ya Arumeru   Emmanuel Kaganda pia katika ziara yake akiongea na wananchi hao  alitoa wito kwa wananchi hao kulima mazao mbadala kama pareto ambalo ndio zao lingine linaloendana na maeneo hayo na kuachana kabisa na kilimo cha bangi ambacho ni hatari kwa wananchi wengine ambao wanaenda Kutumia.



Post a Comment

0 Comments