wachezaji wa Timu ya ASSC A wakiwa na kombe
baada ya kukabidhiwa kombe la mashindano ya Nyerere Cup na mwaka mpya wa
Kiislamu yaliofanyika
Timu ya ASSC A wakisherehekea ubingwa wao baada ya mashindano ya nyerere cup jijini hapa
Bonanza
la mpira wa miguu kusherehekea Mwaka mpya wa
Kiislamu 1439 na kombe la Nyerere 2017 yamefanyika mkoani wa Arusha kwa
siku
mbili na Kuzishirikisha timu kadhaa kutoka Moshi na wenyeji Arusha
katika viwanja ya kiteck nje kidogo ya jiji la Arusha na ASSC kuibuka
bingwa wa mashindano hayo.
Mashindano hayo yalioendeshwa kwa mtindo wa ligi na
kuzishirikisha timu sita kutoka mikoa miwili ya Kilimanjaro na Arusha ambapo
bingwa wa mashindano hayo alikuwa ASSC A kutoka Arusha ambapo alijizolea Pts
10 na kupewa zawadi ya kombe kubwa huku
ndugu zao ASSC B wakishika nafasi ya pili kwa kufikisha pts 10 lakini wakipitwa
kwa uwiano wa magoli waliambulia kombe dogo.
Timu ambazo zilishiriki mashindano hayo ni ASSC A na
B, Al Fur A na B Al Ikhwa na timu kutoka moshi ambapo mashindano hayo
yaliendeshwa kwa mtindo wa ligi hadi kupatikana bingwa
Akiongea mara baada ya kumalizika kwa mtanange huo
ambao ulifanyika kwenye viwanja vya Kiteck nje kidogo ya jiji la Arusha mratibu
wa mashindano hayo Abdul Rab Hanif amesma
kuwa mashindano hayo huwayanafanyika kila mwaka mpya wa kiislamu unapoanza.
Amesema mashindano hayo ya mwaka huu yameenda
sambamba na kumuenzi baba wa Taifa hayati Mwalimu nyerere na kuwa Mwalimu alipenda
kuona mataifa yote hapa duniani na Afrika yanaishi bila kubaguana kwa misingi
ya dini,Kabila wala rangi hivyo ndio maana wameamua kumuenzi kwa michezo.
Alifafanua kuwa Baba wa Taifa alikuwa amejipambanua
kwa kuwa mtu ambaye hakujikweza ndio maana hata sisi leo hatukubagua watu kwa
dini zao wala rangi au kabila kwenye mashindano haya hivyo kila mwaka tutakuwa
tukiazimisha mashindano haya kwa kuita timu kutoka dini tofauti na makabila
tofauti kuweza kuenzi kwa matendo falsafa ya Mwalimu Nyerere.
“Michezo ni Afya na ajira tumekuja kuweka Afya zetu
katika hali inayotakiwa na pia kuvumbua vipaji vipya katika mashindano haya ya
mpira wa miguu ya kumuenzi baba wa Taifa letu”Alisema Hanif.
Bonanza
la mpira wa miguu kusherehekea Mwaka mpya wa
Kiislamu 1439 na kombe la Nyerere 2017 yamefanyika mkoani wa Arusha kwa
siku
mbili na Kuzishirikisha timu kadhaa kutoka Moshi na wenyeji Arusha
katika viwanja ya kiteck nje kidogo ya jiji la Arusha na ASSC kuibuka
bingwa wa mashindano hayo.
Mashindano hayo yalioendeshwa kwa mtindo wa ligi na
kuzishirikisha timu sita kutoka mikoa miwili ya Kilimanjaro na Arusha ambapo
bingwa wa mashindano hayo alikuwa ASSC A kutoka Arusha ambapo alijizolea Pts
10 na kupewa zawadi ya kombe kubwa huku
ndugu zao ASSC B wakishika nafasi ya pili kwa kufikisha pts 10 lakini wakipitwa
kwa uwiano wa magoli waliambulia kombe dogo.
Timu ambazo zilishiriki mashindano hayo ni ASSC A na
B, Al Fur A na B Al Ikhwa na timu kutoka moshi ambapo mashindano hayo
yaliendeshwa kwa mtindo wa ligi hadi kupatikana bingwa
Akiongea mara baada ya kumalizika kwa mtanange huo
ambao ulifanyika kwenye viwanja vya Kiteck nje kidogo ya jiji la Arusha mratibu
wa mashindano hayo Abdul Rab Hanif amesma
kuwa mashindano hayo huwayanafanyika kila mwaka mpya wa kiislamu unapoanza.
Amesema mashindano hayo ya mwaka huu yameenda
sambamba na kumuenzi baba wa Taifa hayati Mwalimu nyerere na kuwa Mwalimu alipenda
kuona mataifa yote hapa duniani na Afrika yanaishi bila kubaguana kwa misingi
ya dini,Kabila wala rangi hivyo ndio maana wameamua kumuenzi kwa michezo.
Alifafanua kuwa Baba wa Taifa alikuwa amejipambanua
kwa kuwa mtu ambaye hakujikweza ndio maana hata sisi leo hatukubagua watu kwa
dini zao wala rangi au kabila kwenye mashindano haya hivyo kila mwaka tutakuwa
tukiazimisha mashindano haya kwa kuita timu kutoka dini tofauti na makabila
tofauti kuweza kuenzi kwa matendo falsafa ya Mwalimu Nyerere.
“Michezo ni Afya na ajira tumekuja kuweka Afya zetu
katika hali inayotakiwa na pia kuvumbua vipaji vipya katika mashindano haya ya
mpira wa miguu ya kumuenzi baba wa Taifa letu”Alisema Hanif.
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia