Ticker

6/recent/ticker-posts

MKURUGENZI MANISPAA YA ILALA JIJINI DAR ES SALAAM ATOA CHETI KWA MTUNZA MALI ZA UMMA


Na Leonce Zimbandu

MKURUGENZI wa Manispaa ya Ilala, Msongela Palela ametoa cheti cha shukurani kwa Mkazi wa Mtaa wa Kichangani kata ya Majohe, Gabriel Macheho (pichani) baada ya kutambua mchango wake wakuhifadhi na kutunza rasilimali za umma. 

Moja ya rasilimali hizo ni pamoja na kusimamia eneo la umma lisichukuliwe na kumilikiwa na watubinafsi, likiwamo eneo  lamachimboyamchangalililokuwalikimilikiwanaMbezi Tile.
Afisa Uhusiano wa Manispaa hiyo, Tabu Shaibu alimkabidhi Macheho cheti hivi karibuni kwa niaba ya Mkurugenzi ili kutoa motisha kwa wananchi wenye moyo wakutoa utetezi wa mali za umma.


Alisema  Manispaa imeamua kutoa cheti hicho baada ya kutambua mchango aliotoa mkazi huyo kwa kufuatilia hadi kufanikiwa kupatikana kwa eneo hilo kwa ajili ya matumizi ya shughuli za kijamii, ikiwamo ujenzi wa soko na shule.

“ Tunapaswa kuonesha uzalendo wakufuatilia mambo yenye manufaa kwa jamii ilikuishaidia jamii inayo kuzunguka,” alisema.

Mkazi wa Majohe Andrew Msuya alisema amefurahishwa na kitendo cha Serikali kutambua mchango wa wananchiwachini,   hiyo italeta chachu kwa watu wengine kuendeleza na kuhifadhi mazingira.
“ Naombaserikalikuendeleakuthaminimchangowawatuwachinikwakutoamotishailikukuzauhusianomzuri,” alisema.

Gabriel Macheho ameishukuru serikali kwa kutambua mchango wake wa kutunza na kuhifadhi rasilimali za umma, kwani wananchi wengi hawakujua kama huo ulikuwa ni wajibu wa msingi kutekeleza.

“Nitaendelea kutoa mchango wangu kwa serikali na jamii kwa ujumla ili kuhakikisha maeneo ya umma yanaendelea kulindwa na kuhifadhiwa,” alisema.



Post a Comment

0 Comments