Ticker

6/recent/ticker-posts

TUNAWATAKIA MWEZI MTUKUFU MWEMA WA RAMADHANI

Mwezi wa 9 katika kalenda ya kiislamu ni mwezi mtukufu wa Ramadhani ambao ni maarufu zaidi kutokana na ibada ya Saumu.
Katika mwezi huu waislamu hutakiwa kufunga kutoka Machweo mpaka Machwa (Mawio) katika kipindi ambacho hawatakiwa kula wala kunywa chochote.
Mwezi wa Ramadhani ni muhimu kwa waumini was dini ya kiislamu kwa kuwa ndio mwezi ulioteremshwa Kurani na pia hufahamika kama mwezi wa Kurani.
Mbali na kujiepusha na kunywa na kula Muislamu hutakiwa kujiepusha na maovu na matendo ya dhambi na kuongeza katika matendo ya ibada kama Swala, Kusoma Kurani, kutoa sadaka na kadhalika.
Katika nchi nyingi duniani mwezi huu unaanza hivi leo tarehe 27 mwezi Mei mwaka wa 2017.
Ramadan Mubaraq
Mathias Canal
0756413465
Dar es salaam

Post a Comment

0 Comments