Ticker

6/recent/ticker-posts

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YATOA SEMINA KWA WABUNGE JUU YA UMUHIMU WA UHIFADHI WA MALIASILI, MALIKALE NA MAENDELEO YA UTALII NCHIN


Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Mhandisi Atashasta  Ndetiye (kushoto) akizungumza wakati wa semina hiyo iliyoandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii na kufanyika katika ukumbi wa Bunge mjini Dodoma jana. Kulia ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Prof. Jumanne Maghembe. Semina hiyo ilihusu umuhimu wa uhifadhi wa Maliasili Malikale na Maendeleo ya Utalii nchini.
Baadhi ya viongozi na watumishi wa Wizara ya Maliasili na Utalii wakiwa ndani ya ukumbi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania muda mfupi kabla ya kuanza kuwasilishwa kwa mada mbalimbali katika semina hiyo. Mada zilizowasilishwa katika semina hiyo ni Kwanini Watanzania tuhifadhi uoto wa asili na Wanyamapori, Athari za Muingiliano wa Mifugo na Wanyamapori, Maendeleo ya Utalii na umuhimu wake katika uchumi wa Tanzania na Umuhimu wa Uhifadhi wa Misitu Nchini.
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Meja Jeneral Gaudence Milanzi akizungumza katika semina hiyo iliyoandaliwa na Wizara kwa ajili ya wabunge wote wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mkurugenzi wa Idara wa Wanyamapori wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Prof. Alexander Songorwa askiwasilisha mada kuhusu umuhimu wa Watanzania kuhifadhi uoto wa asili na Wanyamapori katika semina hiyo. Kushoto waliokaa ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe na baadhi ya viongozi na wakurugenzi wa Wizara ya Maliasili na Utalii.
Prof. Songorwa akiwasilisha mada hiyo. 
Mkurugenzi wa Kituo cha Utafiti wa Wanyamapori katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Dkt. Robert Fyumagwa akiwasilisha mada juu ya Athari za Muingiliano wa Mifugo na Wanyamapori katika semina hiyo.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania, Prof. Dos Santos Silayo akiwasilisha mada juu ya Umuhimu wa Uhifadhi wa Misitu Nchini. Alieleza kuwa umuhimu wa misitu ni sawa na hewa safi ambayo inatoa uhai kwa mwanadamu na endapo misitu hiyo itatoweka kutokana na uharibifu unaoendelea basi maisha ya binadamu nayo yatakuwa hatarini kwa kuwa hewa hiyo chanzo chake ni misitu na mimea.
Katibu Mtendaji wa Shirikisho la Vyama vya Utalii Tanzania, Richard Rugimbana akiwasilisha mada kuhusu Maendeleo ya Utalii na umuhimu wake katika uchumi wa Tanzania kwa wabunge hao.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe na Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Mhandisi Atashasta  Ndetiye (kushoto) wakifuatilia mada zilizokuwa zikiwasilishwa katika semina hiyo.
Aliyekuwa MC wakati wa semina hiyo, Meneja wa Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania, Paschal Shelutete akiteta jambo na Mbunge wa Kigoma Mjini, Zito Kabwa muda mfupi baada ya kuhitimishwa semina hiyo.
 Baadhi ya viongozi wa Wizara ya Maliasili walioshiriki semina hiyo bungeni mjini Dodoma.
Bungeni wakati wa semina hiyo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (wa pili kushoto), Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Mhandisi Stella Manyanya (wa pili kulia), Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori Wizara ya Maliasili na Utalii, Prof. Alexander Songorwa na Mkurugenzi wa Idara ya Misitu Wizara ya Maliasili, Dkt. Ezeckiel Mwakalukwa wakitoka katika ukumbi wa bunge mara baada ya semina hiyo.

Post a Comment

0 Comments