Ticker

6/recent/ticker-posts

WAMUOMBA WAZIRI TAMISEMI SIMBACHAWENE KUNUSURU KAYA ZAO



Na Woinde Shizza, Kondoa
Wafanyakazi wa Halmashauri ya wilaya ya Kondoa dc idara za Ulinzi,Madereva,watendaji Kata na vibarua wanaolipwa kwa fedha za makusanyo ya mapato ya ndani wamemuomba waziri wa Tamisemi George Simbachawene kunusuru kaya zao kwa kuingilia kati suala lao la malimbikizo ya mishahara wanaoidai  kwa miezi mitano sasa ili kuwanusuru na hali ngumu ya kimaisha wanaokabiliana nao kwa sasa.

Wafanyakazi hao waliongea na gazeti hili wilayani humo nakusema  kuwa wanakumbana na  hali ngumu ya kimaisha inayosababishwa na wao kukosa fedha zao za mishahara kwa miezi mitano sasa huku wimbo ukiwa ni suala lao lipo kwenye mchakato na miezi inaenda.

Mmoja wa wafanyakazi aliekataa kutaja jina kwa hofu ya kusimamishwa kazi kwenye idara ya ulinzi alisema kuwa wamekuwa wakifuatilia fedha zao kwa kipindi kirefu huku wakiambiwa mkurugenzi amekwisha saini dodoso la malipo yao lakini wao mpaka leo hawajalipwa chochote hiyo imekuwa ikiwawiya vigumu katika hali za kimaisha mjini.
Amesema kuwa mjini unakuwa umepanga nyumba una watoto unasomesha wanahitaji chakula na mahitaji mengine sasa unafikiria utaishi vipi kwa hali tunamuomba waziri Tamisemi kuingilia kati kuweza kulipwa fedha zetu kwani mamlaka zote ngazi ya wilaya wanalijua suala letu bila majibu wala kupata stahiki zetu tena ambazo tunazivujia jasho usiku na mchana.

Kwa upande wake mmoja wa vibarua amesema kuwa fedha zao wanazodai katika halmashauri hiyo imekuwa ni usumbufu na kila wanapokwenda kwa Mhazini wa halmashauri madai yake fedha hakuna fedha hivyo wao kuendelea kuishi katika hali ngumu ya kimaisha na huku familia zikiwategemea.

“Sisi tunamuomba sasa waziri simbachawene kulifuatilia suala letu kwani tunaimani na serikali ya awamu ya tano katika kuwajali wanyonge na watu wa kipato cha chini hivyo tunaamini atalishughulikia”aliongeza mfanyakazi huyo






Post a Comment

0 Comments