wananchi wakiwa nje ya uwanja mara baada yakushindwa kuingia ndani kutokana na wingi wa watu
miili ya marehemu ikiwasili katika kiwanja cha kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid tayari kwa zoezi la kuagwa
mmoja wa mwanafunzi akiwa
amebebwa na wahudumu wa chama cha msalaba mwekundu mara baada ya
kuzidiwa na kuanguka ndani ya uwanja wa Sheikh Amri Abeid wakati
alipokuja kuaga wanafunzi wenzake (picha zote na Woinde Shizza,Arusha)
Na Woinde Shizza,Arusha
MAKAMU wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa taTanzania Samia
Suluhu ameongoza maelfu ya waombolezaji katika zoezi la kuaga miili ya
wanafuzi 35 wa shule ya Luck Vicent ikiwemo walimu wawili pamoja na
dereva mmoja waliofariki katika ajali iliyotokea juzi eneo la Rotia
wilayani karatu mkoani Arusha.
Akizungumza katika tukio
hilo ambalo ni kubwa kutokea mkoani arusha na tanzania kwa ujumla
alisema kuwa kama serikali walmelipokea kwa masikitiko makubwa na kwamba
watajitahidi kuungana na familia zilizopoteza watoto wao ambao hata
wazazi wao walikuwa na malengo mazuri juu ya kuwapatia elimu bora ,huku
akiwaagiza madereva wote kuzingatia sheria za barabarani na kuepuka
vilevi.
Alisema kuwa ajali nyingi zinatokana na uzembe
wa madereva na hivyo kuwataka madereva wote kuwa makini pindi wanapokuwa
wakiendesha vyombo vya moto ili kuepuka ajali ambazo zinqweza
kuzuilika.
"Serikali yetu kwa sasa inapiga vita sana
madereva walevi pindi wanapokuwa wanaendesha vyombo vyao hivyo naomba tu
kuagiza madereva wetu kuwa makini na waadilifu kwani hata ajali kama
hizi ambazo zinapoteza nguvu kazi zinatokana na vilevi vinavyotumiwa na
madereva na hivyo kuleta maafa kama haya"aliongeza Samia.
Aidha
aliwataka pia madereva kuhakikisha wanabeba idadi ya watu wanaolingana
na uhalisia wa gari kwani wengi wao wamekuwa wakibeba idadi kubwa na
hivyo kusababisha madhara mkubwa zaido pindi ajali zinazotokea mfano wa
ajali hii.
Samia alitumia fursa hiyo kuiagiza Wizara ya
elimu ,jeshi la polisi kuwa makini kuhakikisha sheria za barabarani
zinazingatiwa ili kuepuka vifo vya watoto.
Awali mara
baada ya kuwasili kwa miili hiyo 35 majira ya saa tano na robo
uwanjani hapo Vilio ,majonzi na simanzi vilitawala katika uwanja huo
huku watu mbali mbali wakiwemo wanafunzi wa shule wakiwa wanazimia na
kuwahishwa mahospitalini ili kupatiwa huduma ya kwanza.
Aidha
katika zoezi hilo la kuaga miili ya wanafunzi hao serikali ya mmkoa wa
arusha ikiongozwa na mkuu wa mkoa huo Mrisho Gambo imeweza kugaharamia
shuguli zote za mazishi ya wanafunzi hao ikiwa ni pamoja na kutoa magari
ya kusafirisha miili hiyo mpaka eneo ambalo familia imejiwekea
utaratibu wa kuhifadhi miili hiyo ambapo miili 25 itasafirishwa nje ya
mkoa wa arusha,huku miili 10 ikibaki kwa taratibu za mazishi ndani ya
mkoa huu.
Hata hivyo akiongoza misa ya kuaga miili hiyo
kwa upande wa wakristo Askofu wa kanisa la katoliki jimbo la arusha
Josphat Lobulu alisema kuwa siku za mwanadamu ni chache hivyo inawapasa
wanadamu kuishi maisha ambayo yanaendana na mapenzi ya Mungu.
Alisema
kuwa vifo vya wanafunzi hao kimesikitisha kila mtu kwa kuwa wamekufa
wakiwa malaika wa Mungu wakiwa bado wanahitajika na taifa la sasa.
Hata
hivyo zoezi hilo la kuagwa kwa miili hiyo limeudhuriwa na viongozi
mbali mbali kutoka serikalini na nje ya nchi wakiwemo waziri wa elimu wa
tanzania ,waziri wa elimu kutoka nchini kenya,jaji mkuu wa mahakama
,jaji mstaafu ,waziri mstaafu lowasa na Sumaye ,viongozi wa kambi ya
upinzani bungeni,madaktari kutoka nje ya nchi pamoja na wabunge mbali
mbali.
Aidha tukio hili lilitokea mei 6 wilayani karatu
ambapo wanafunzi hawa walikuwa wanenda kufanya mitihaninya ujirani mwema
katika shule ya Tumaini na ndipo costa ilifeli breki na kusababisha
vifo 35 na majeruhi watatu ambao ni Doreen Mshana (13),Sadia Ismaili
(11) pamoja na Wilson Tarimo (11)wote wakazi wa Morombo ambapo wote
wamelazwa katika hospitali ya mkoa ya Mount meru wakiendelea na
matibabu.
umati wa watu ukiwa unalia kwa uchungu
Mbunge wa viti maalumu Amina Mollel akiwa analia kwa uchungu mara baada ya kuaga miiili ya marehemu hao
Kaimu Mkuu wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi Ndg:Jokate Mwengeloakiwa anatoa heshima za mwisho mbele ya majeneza yaliobeba miiili ya wanafunzi hao
zoezi la kuaga mwili likiendelea huyu ni mmiliki blog ya fatherkidevu nae akitoa heshima za mwisho
picha za majeneza ya wanafunzi hao 32 pamoja na walimu na dereva aliyekuwa anaendesha gari hilo
umati wawatu uliouthuria katika zoezi la kuaga marehemu hao
mmoja wa Mama aliofiwa na mtoto wake akiwa analia kwa
uchungu mara baada ya miili ya watoto hao kuanza kuwasili katika kiwanja
cha kumbukumbu ya sheikh Amri Abeid
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia