Ticker

6/recent/ticker-posts

NGOMA AFRICA BAND KUTINGISHA ONYESHO KUBWA LA INTERNATIONAL AFRIKA EXPO FESTIVAL TUBINGEN,UJERUMANI JUMAMOSI 3 SEPTEMBER 2022.TUEBINGEN ,GERMANY






Mwanamziki Kamanda Ras Makunja na mzimu wake Ngoma Africa Band
 Mziki wa dansi Kutoka Uswahili hadi kimataifa Ujerumani na ulaya,


Tunapozungumzia muziki dansi wa Tanzania "Bongo Dansi" kuvushwa na kufikishwa katika majukwaa ya kimataifa jina la mwanamuziki mtanzania Kamanda Ras Makunja na bendi yake The Ngoma Africa Band hatuwezi kulikwepa.
 
Mwanamuziki wa kitanzania kamanda Ras Makunja mtunzi,mwimbaji,kiongozi na mwanzilishi wa bendi maarufu Ngoma Africa band aka FFU au viumbe wa ajabu "Anunnaki Aliens" yenye makao yake nchini ujerumani,bendi inayodumu
 
kwa takribani miaka 29 tangu aianzishe mwaka 1993 kwa madhumuni ya kuitangaza nchi Tanzania kimataifa kwa kupitia njia ya muziki wa dansi na kujizolea washabiki na tuzo za kimataifa,ikiwepo tuzo ya bendi bora ya kigeni iliyodumu kwa muda mrefu barani ulaya "Best Diaspora Band Award" sio jambo rahisi kwa bendi ya kigeni tena ya kiafrika kuweza kuimili na kudumu kwa zaidi miongo miwili barani ulaya na bendi nyingi za kigeni zimeshindwa kutimiza hata mwaka moja lakini mtanzania mwamba huyu Ras Makunja ameweza kuongoza mzimu wake Ngoma Africa Band na kufanikiwa kuwanasa malfu ya washabiki na kuitangaza Tanzania.
 
 
Mwanamuziki huyu Kamanda Ras Makunja ni nani haswa ?
mwanamuziki mwamba huyu nguli jina lake haswa alilopewa na wazazi wake ni
Ebrahim Jumanne Salehe Makunja alizaliwa Dar es salaam ni mtoto wa mwanzo wa Bw.Jumanne Salehe Makunja na Bi.Mozah Hassan Mpili.


  inasemekana wazazi wake walimpeleka kupata elimu akiwa na umri mdogo katika shule ya kinondoni,osterbay na elimu ya kati Kibasila na kupata mafunzo ya masoko na biashara katika tahasisi ya Impex iliyopo Birmingham uingereza na baadaye North-West Europe business Zentrum kule Heldesheim ,Ujermani,anaongea lugha nne za kimataifa Kijerumani,Kingeleza,Patois na kiswahili kutokana na vipawa hivi wenzetu wa jerumani walimgundua kuwa huyu ni madini wakampa ugali wa kuwa mtaalam anayeshughulikia 
 Conseling kwa watoto na vijana katika kituo cha JugendKultur Zentrum katika mji wa Oldenburg kituoa ambacho kinatoa ushauli kwa watoto na vijana katika shughuli za sanaa,elimu na muziki,ambapo alifanikiwa kuifanya kazi ya kuokoa vijana zaidi ya elfu sita walikuwa wanasumbua mitaani baada ya shule katika mji wa Oldenburg,kazi ambayo polisi wa jiji walishindwa kuifanya kwa ajili ya kutumia nguvu lakini Kamanda Ras Makunja aliifanya kwa kutumia mbinu ambazo wajerumani waliziita (Psychologist) na kumtaja mwamba huyu kuwa ni kiumbe wa ajabu the Alien mwenye mvuto wenye ushawishi mkubwa.
 
 
Ras Makunja ni mume na baba familia yake ni kitanzania,Ras Makunja bado raia wa Tanzania pamoja na kuwa mara nyingi ameombwa kuwa raia wa ujerumani lakini amekataa anaishi ujerumani kwa muda wa miaka 28 sasa na kupata hati ya mkazi wa kudumu.
 
 
Safari yake ya maisha ya muziki ilianzia mapema sana akiwa na umri mdogo
akiwa katika vikundi vya kwaya ya shule na kufanikiwa katika umri mdogo akiwa shuleni kinondoni kujiunga na kwaya maarufu wakati huo ya Umoja wa Vijana wa chama cha TANU (TYL) Tanu Youth League iliyokuwa inaongozwa na mzee Makongoro,kwaya hiyo ilikuwa na utaratibu wa kuchukua watoto wenye vipaji kutoka mashuleni na kuimba nao,lakini wazazi wa 
Makunja walikuwa makini na wakali sana katika kuhakikisha mtoto wao anapata elimu ya kutosha kuliko kutekwa na sanaa ya muziki na walifanikiwa katika hilo,pamoja na hayo mtoto wao yaani kamanda Ras Makunja naye alifanikiwa ndoto yake ya muziki mwaka 1978 alijiunga kwa muda mfupi na Butiama Jazz iliyokuwa inamilikiwa na marehemu Mustafa Mkwega baadaye alitoka kutokana na alipata ajira iliyokuwa
ngumu kugawa muda wa muziki na kazi,ajila hiyo ilikuwa kati ya Mazimbu Morogoro na Dar Es Salaam kuudumia wapigania uhuru wa kusini mwa afrika.
 
Baadaye alijiunga na kundi la Roots and Culture liliongozwa na marehemu Jah Kimbute Mleteni bendi ambayo nayo ilitumika sana katika harakati za kupigania uhuru wa kusini mwa afrika,bendi hiyo ndiyo iliyokuwa inazungua katika nchi sita zilizo mstali wa mbele (Frontline States) bendi hiyo nayo iliweza kutembea katika kila nchi na kuwafikiwa wapigania uhuru na kuwatia hamasa.
Ras Makunja kuanzia 1990 alipaata fursa ya kuanza kusoma kijerumani Goithe Institut Dar na kupata fursa ya kuchaguliwa katika timu  watafiti iliyoundwa na wajerumani na watanzania kuhusu utamaduni na utalii (Tourist Impact of Tanzania).
 
baadaye akaondoka katika kundi la muziki la Roots and Culture na kuhamia nchini Ujerumani kujiendeleza kielimu na akafanikiwa kuanzisha bendi yake Ngoma Africa Band mwaka 1993 ikapata udhamini wa project ya "We are One" wazunguka kupiga muziki Ujermani yote kwa kupinga ubaaguzi wa rangi ambao miaka ya 1990s ulikuwa umeshika kasi.makunja na bendi yake walifanikiwa kubadilisha fikira za vijana wa kijerumani wengi kwa kupitia silaha ya muziki wa dansi ambao hapa Tanzania hauna thamani.
 
Mwaka 2000 aliingoza bendi yake katika maonyesho ya World Expo 2000 Hannover, tarehe 8.08.2000 katika malumbano ya jukwaani mwamba Kamanda Ras Makunja na bendi yake aliipaisha Tanzania kimataifa na kuchaguliwa kuwa The Best Worldmusic band of Expo 2000 Hannover.mwaka 2001 Makunja aliongoza bendi yake at "Pacific World Music Festival Honolulu,Hawai.
 
Mwaka 2007 Fiesta Latina ,Caracas Venezuela.Mwaka 2010 Ras Makunja na mzimu wake ndani ya Finland, mwaka 2011 Ras Makunja na bendi yake akaingia Serbia,Bosnia ambako si nchi rahisi kutokana kuwa nchi hizo zilikuwa zimetoka kwenye vita,mwaka huo huo 2011 Kamanda Ras Makunja na bendi yake walipata mwaliko wa kwenda Libya lakini serikali ya Ujerumani ilizuia bendi hiyo kwani hali ya Libya haikuwa shwali.Mtanzania huyu Ras Makunja mwaka 2014 na bendi yake walialikwa kwenda kutumbuiza katika sherehe za miaka 60 ya taifa la Israeli wakafanikiwa kutingisha katika uwanja wa Isaack Rabin Square mjini Tel-Aviv.
 
Kamanda Ras Makunja mkuu wa kikosi maalumu The Ngoma Africa Band au the FFU-Ughaibuni almaarufu pia kama viumbe wa ajabu "Anunnaki Aliens" akipanda jukwaani ni kazi moja tu kuwadatisha maelfu ya washabiki katika maajukwaa ya kimataifa na kuipeperusha tanzania.Ras Makunja mwimbaji,mtunzi pia social commentator mwenye kutunga nyimbo za kuelimisha na kugusa jamii zikiwe CDs kama "Rushwa Ni adui wa Haki"
 
 CD:Mama Kimwaga ,CD: Apache wacha Pombe, CD;Miaka 50 ya Uhuru
na nyingi nyinginezo.Kamanda Ras Makunja mtoto wa Tanzania aliyejitoa muanga kuipeperusha bendera ya Tanzania kimataifa.



 

Post a Comment

0 Comments