mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Arusha mrakibu wa Polisi SP SOLOMON MWANGAMILO akiongea na baadhi ya askari WA usalama barabarani mara baada ya kutoa elimu kwa madereva zaidi ya mia moja (100) na kuwakumbusha madereva wa mabasi yaendayo mikoani kutii sheria za usalama barabarani ili kupunguza ajali kama sio kumaliza kabisha ajali za barabarani katika mkoa wa Arush elimu hiyo wameitoa katika stand kuu ya mabasi yaendayo mikoani na nchi Jirani ambapo amesema kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Arusha kimejipanga vyema kudhibiti ajali katika mkoa wa Arusha
Na. Abel Paul wa Jeshi la Polisi mkoa wa Arusha.
Jeshi
la Polisi mkoa wa Arusha kupitia kikosi cha usalama Barabarani mkoa wa
Arusha kimetoa elimu kwa madereva Zaidi ya mia moja (100) na
kimewakumbusha madereva wa mabasi yaendayo mikoani kutii sheria za
usalama barabarani ili kupunguza ajali kama sio kumaliza kabisha ajali
za barabarani katika mkoa wa Arusha.
Hayo
yamesemwa leo agosti 16 2022 na mkuu wa kikosi cha usalama barabarani
mkoa wa Arusha mrakibu wa Polisi SP SOLOMON MWANGAMILO katika stand kuu
ya mabasi yaendayo mikoani na nchi Jirani ambapo amesema kikosi cha
usalama barabarani mkoa wa Arusha kimejipanga vyema kudhibiti ajali
katika mkoa wa Arusha.
Mwangamilo
amesema kuwa ajali nyingi zimekuwa zikisababishwa na mwendokasi pamoja
na kuyapita magari mengine bila kuchukua tahadhari (overtaking) ambapo
ameeleza kuwa vitendo hivyo vimekuwa vikiacha simanzi kwa familia,ndugu
na jamaa ambao upoteza wapendwa wao kwa uzembe wa baadhi ya madereva
wasiofuata sheria za usalama barabarani.
SP
Mwangamilo ameeleza kuwa katika siku za hivi karibu kumejitokeza tabia
ya madereva kukiuka taratibu nasheria za usalama barabarani na kuendesha
magari hayo mwendo kasi ambapo amesema kuwa dereva atakaye kamatwa
akikiuka sheria hizo atakamatwa na kufungiwa leseni yake kwa kipindi cha
miezi mitatu hadi sita.
Nao
baadhi ya madereva wa mabasi yaendayo mikoani wamelishukuru Jeshi la
Polisi mkoa wa Arusha hususani kikosi cha usalama barabarani mkoa wa
Arusha kuendelea kutoa elimu kwa madereva mara kwa mara ili kuwajengea
uwezo na umahiri ili kupunguza ajali ambazo zinaweza kuepukika.
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia