BREAKING NEWS

Friday, August 5, 2022

TEMDO YAMLETEA MKULIMA SULUISHO LA KUSAFISHA MAFUTA GHAFI BAADA YA KUBUNI MTAMBO WA KUSAFISHA MAFUTA YA ALIZETI


Ofisa wa Kitengo cha Mawasiliano na Masoko Dkt. Sigisbert Mmasi kutoka Taasisi ya ubunifu na Usanifu mitambi Tanzania (TEMDO)akielezea jinsi mashine ya kusafisha mafuta ilivyokuwa kivutio ndani ya maonyesho ya nane nane yanayofanyika katika viwanja vya themi njiro ndani ya halmashauri ya jiji la Arusha ambapo alisema mashine huyo ni Moja ya miradi yao 16 mipya iliopo katika taasisi yao na nimkombozi Kwa mkulima wa alizeti


Na Woinde Shizza , ARUSHA 

Taasisi ya uhandisi na usanifu mitambo nchini (TEMDO) imebuni mtambo mpya wa kisasa wa kusafisha mafuta ya alizeti   kwa kiwango cha juu kwa ajili ya matumizi  salama ya binadamu.


Taasisi hiyo imeutambulisha mtambo huo kwa mara ya kwanza Kwa mikoa ya Kanda ya kaskazini  katika maonyesho ya 28 ya sikukuu za wakulima nchini (Nane Nane) yanayoendelea katika viwanja vya Themi  Njiro  ndani ya halmashauri ya jiji Arusha.



Akizungumza na waandishi wa habari mkuu wa kitengo cha mawasiliano na masoko katika taasisi hiyo,dkt Sigisbert Mmasi alisema katika maonyesho haya ya nane nane wameweza kuleta teknolojia nne ambazo hawajawahi kuzileta katika maonyesho hayo ambazo ni mtambo wa kuchakata mafuta ya alizeti ambao unaanzia kwenye mashine ya kupokea mbegu unafata mashine ya kukamua mafuta,ukisha kamua unaenda kwenye mashine  ya kuchuja ukisha maliza kuchuja ndio unaenda kwenye mtambo Kwa ajili ya kusafisha mafuta hayo.


" Unajua ukiangalia mafuta mengi yanayouzwa uko mtaani unakuta yamekamuliwa na mkulima  na kuchujwa na kuuzwa apo apo na muda mungine unakuta mtu anasifia mafuta hayo kwakuwa ameona yanavyo kamuliwa lakini mafuta yale yanakuta sio mazuri bila ya kusafisha kwasababu yanakuwa bado nimafuta ghafi,nikisema ghafi ni mafuta ambayo ndani yake yana kitu kama gundi ,uchafu pamoja na vitu vingine ambavyo vina athari Kwa afya ya binadamu"alisema Mmasi

 


Alisema kwamba mtambo huo utasaidia kusafisha mafuta ghafi ya alizeti ambayo yana athari kwa afya ya binadamu na kuyasafisha katika ubora unaoitajika  huku akiwataka wakulima kuwekeza katika mtambo huo kwa manufaa ya biashara zao na afya ya mlaji



Sambamba na mtambo huo mitambo mingine iliyobumiwa na taasisi hiyo ni ,mtambo wa kuchakata Sukari,mtambo wa kukamua mafuta ya Parachichi, vifaa tiba ambavyo Kiteketezi taka hatarishi za hospitali za hospitali ,  Vitanda vya kujifungulia wa Mama Wajawazito, Vitanda vya kukagulia na Kulazia Wagonjwa,stand ya drip , jokofu la kuhifadhia maiti pamoja kabati la kuifadhia vitu vya mgonjwa ambapo alibainisha kuwa Kwa sasa TEMDO inavifaa Tiba vyenye ithibati zaidi ya kumi na tano (15) vyenye ithibati ya TMDA.


Alisema lengo kuu la kutengeneza Vifaa Tiba ni pamoja na   kuweza kusaidia  kupunguza matumizi ya fedha za kigeni kuagiza nje ya nchi, kuongeza ajira za ndani na kurahisisha upatikaniji wa bidhaa kirahisi na kwa bei nafuu


Akiongelea mtambo wa kuchakata sukari alisema kuwa mtambo huu utasaidia sana kuongeza ajira Kwa watanzania pia itasaidia kupunguza tatizo la masoko Kwa wakulima wa miwa kwani Kiwanda kitakuwa na uwezo wa kuchakata Tani 20 za Sukari kwa Siku ambazo ni sawasawa na Tani 200 miwa

 


Awali akiongea katika maonyesho hayo mkuu wa wilaya ya Arumeru, Mhandisi Richard Ruyango alizitaka taasisi za kilimo kubuni zana mbalimbali zitakazowasaidia wakulima katika shughuli zao ambapo aliipongeza taaisisi ya Temdo kwa ubunifu wa mitambo mbalimbali itakayosaidia maendeleo ya kilimo, mifugo na uvuvi nchini .




Alifafanua  kuwa, maonyesho hayo yanatarajiwa kuchangia ukuaji wa mabadiliko kwa wakulima kutoka maeneo mbalimbali endapo elimu ya kutosha itatolewa na kuenea kwa kwa jamii inayowazunguka juu ya kilimo na ufugaji wa kisasa ambapo pia  aliwataka watalaamu wa kilimo nchini kuendelea kutoa elimu ya kutosha kwa wakulima na wafugaji ili walime na kufuga kisasa na kuepukana na kuondokana na zana za zamani na hatimaye kuweza kubadilisha maisha yao.


Naye Mkuu wa wilaya ya Kiteto ,Mbaraka Alhaji Yusuph alisema kuwa,maonyesho hayo yameshirikisha waonyeshaji 200 kutoka Taasisi mbalimbali licha ya taarifa kuchelewa juu ya uwepo wa maonyesho,lakini mwitikio bado ni mkubwa sana.


Alitaja kaulimbiu ya maonyesho hayo Kwa mwaka huu kuwa ni "kilimo ni biashara ,shiriki kuhesabiwa Kwa mpango bora ya kilimo ,mifugo na uvuvi"ambapo aliwasiitiza wananchi  Kushiriki katika zoezi la sensa .



Share this:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

 
Back To Top
Copyright © 2014 MOUNT KILI NEWS. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates