BARAZA LA MADIWANI HALMASHAURI YA MERU LAGOMA KUPOKEA TAARIFA ZA KATA AMBAZO HAZIJAFUATA UTARATIBU

 
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Will J. Njau  wakati wa ufunguzi wa mkutano wa robo ya 3 wa baraza la Halmashauri hiyo amesema mbali na  changamoto ndogo ndogo zilizopo kwenye Halmashauri hiyo ,Mwenendo wake unaridhisha kwani ukusanyaji wa mapato  umefikia asilimia 68.2 kiasi ambacho ni cha juu ikizingatia kuna vyanzo kama 3 vilivyotwaliwa na Serikali kuu  kikiwemo ushuru wa mabango, pia Halmashauri hiyo  imezawadiwa gari kwa kufanya vizuri kwenye Usafi na Mazingira , pia imeshika nafasi nzuri kwenye ufaulu wa shule za sekondari na msingi .
Baadhi ya wajumbe ambao ni madiwani wamelalamikia kitendo cha fedha za miradi ya maendeleo kutokupelekwa jambo linalosababisha miradi mingi kusimama kwenye Kata  ambapo makamu mwenyekiti  wa Halmashauri  hiyo,Nelson Mafie ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya fedha ,mipango na utawala amewashauri wajumbe hao kujiridhisha kama miradi wanayoisemea ipo kwenye bajeti.
Nae Kaimu mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Dkt.Amani Sanga amefafanua kuwa kwa mwaka wa fedha 2017/2018 Halmashauri hiyo ilipitisha kwenye bajeti yake fedha kutoka mapato yake ya ndani kiasi cha Biliono 2,226,374,000 kwa ajili ya miradi ya maendeleo hadi sasa zaidi ya milioni 350,270,430 ya fedha  hizo imepelekwa kwenye miradi ya maendeleo ,pia amesema fedha zinazopelekwa kwenye miradi ya maendeleo hutegemea ukusanyaji wa mapato.
Aidha mkutano huo wa baraza la Halmashauri ya Wilaya ya Meru ambao ni wa siku 2  umehairishwa kwa siku  ya kwanza ukiwa na azimio kuwa halitapokea taarifa za utekelezaji wa kata ambazohazija fuata utaratibu wa kisheria wa kujadiliwa na kupitishwa kwenye baraza la maendeleo ya Kata (WDC) .

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

Previous Post Next Post