Ticker

6/recent/ticker-posts

DKT,MAHIGA ATEMBELEA TAASISIS YASAVE THE CHILDREN HAERT YA ISRAEL

zao. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe, Dkt. Augustine Mahiga (kushoto) akimjulia hali mmoja wa watoto kutoka Tanzania anayepata tiba ya maradhi ya moyo katika Taasisi ya Moyo ya Save the Children Heart ya Israel 
Kutoka kulia, mtu wa kwanza na wa pili ni Watanzania wanaosomea fani za tiba za maradhi ya moyo katika taasisi ya Save the Children Haert wakiongea na Mhe. Waziri wakati alipoitembelea taasisi hiyo jijini Tel Aviv, Israel leo. 
Mkurugenzi wa Taasisi ya Save the Children Heart ya Israel akitoa maelezo kwa Mhe. Waziri hayupo pichani namna taasisi hiyo inavyofanya kazi. 
Wanne kutoka kushoto ni wanafunzi kutoka Tanzania wanaosomea fani ya tiba ya maradhi ya Moyo wakimsikiliza Mkurugenzi wao hayupo pichani. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe, Dkt. Augustine Mahiga (kushoto) akimkabidhi zawadi Mkurugenzi wa Taasisi ya Save the Children Heart/ 
Kaimu Mkurugenzi wa Mashariki ya Kati kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Suleiman Salehe akibadilishana mawasiliano na wanafunzi wanaosomea fani ya tiba ya maradhi ya moyo kutoka Tanzania. 
Ulinzi wa Mpaka kwenye Ukanda wa Ghaza 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe, Dkt. Augustine Mahiga (kushoto) akisalimiana na Afisa Usalama kutoka Kitengo cha Protection Unit alipowasili katika eneo la Netiv Haasara lililopo Ghaza ambapo ni mpakani na eneo la Palestina linalotawaliwa na Hamas. 
Mkazi wa eneo la Netiv Haasara, Ghaza, Bibi Hila Fenton akitoa maelezo kwa Mhe. Waziri na wajumbe wengine kuhusu madhila wanayokutana nayo wananchi wa Israel wanaoishi karibu na mpaka wa Ghaza. 
Bibi Hila Fenton akionesha mabaki ya gruneti la kwanza kabisa kurushwa kutoka Palestina na kuangukia kwenye eneo wanaloishi mwaka 2001/ 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe, Dkt. Augustine Mahiga (kushoto) akipokea maelekezo alipowasili eneo la mpaka katika ukanda wa Ghaza lililojengwa ukuta/ 
Wageni wanaofika katika eneo la mpaka huu wanaombwa kuandika ujumbe wa matumaini katika mawe yaliyotengenezwa kwa sanaa ya aina yake na kuyabandika kwenye ukuta unaozuia maguruneti kupita. Hapo Mhe, Waziri na Balozi wa Tanzania nchini Israel, Mhe. Job Masima wakibandika vijiwe vyenye ujumbe wa kuleta matumaini kwenye ukanda wa Ghaza. 
Bi. Kisa Mwaseba naye akibandika ujumbe wake 
Sehemu ya ukuta wa sengenge unaotenganisha mpaka wa Israel na Palestina katika Ukanda wa Ghaza. 
Sehemu ya ukuta uliojengwa imara kuzuia vijiji vya Israel vilivyo mipakani visifikiwe na mashumbulizi ya magruneti. 

Eneo la Ukaguzi wa Malori ya mizigo
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akipata maeleozo kutoka kwa Meneja wa Usalama wa ukaguzi wa malori ya mizigo yanayokwenda Palestina kutoka Israel na kinyume chake. 
Meneja wa Usalama anatoa maelezo namna kazi ya kukagua malori ya mizigo inavyofanywa kwa uangalifu mkubwa ili kuzuia uwezekano wowote wa kupitisha vilipuzi au vifaa vya kuundia vilipuzi. 
Baadhi ya Malori ya mizigo
baadhi ya mizigo ambayo imekamilika kukaguliwa inasubiri kusafirishwa
Eneo la ukaguzi wa maslori ya mizigo ambalo pia limejengewa ukuta kwa ajili ya kuzuia mashambulizi ya maguruneti. 
Scanner inayotumika kukagua malori ya mizigo ambayo ina nguvu kubwa ya kubaini vifaa vilivyobebwa katika lori kimoja baada ya kingine. kutokana na nguvu ya scanner hiyo harusiwi mtu kukaa karibu inapofanya kazi. 
Waziri Mahiga akionesha moja ya mitambo iliyofungwa kwa ajili ya kuzuia bomu lisilipuke kabla halijasababisha madhara. 


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga ameshukuru Ushirikiano kati ya Taasisi ya Moyo ya Save the Children Heart ya Israel na Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete kwa kuokoa maisha ya watu wengi nchini, hususan watoto.

Waziri Mahiga alitoa shukrani hizo leo alipoitembelea taasisi hiyo jijini Tel Aviv, Israel akiwa anaendelea na ziara yake ya siku tatu aliyoianza jana. "Zamani nilijua kuwa mtu akizaliwa na maradhi ya kurithi, mtu huyo hawezi kuishi lazima atakufa, lakini uwepo wa taasisi yenu kumenifanya niondoe itikadi hiyo" Dkt. Mahiga alisema.

Taasisi ya Moyo ya Save the Children Heart imeisifu Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete kuwa ni moja ya Taasi bora kusini mwa Jangwa la Sahara na kwamba ina uwezo na wataalam wa kufanya upasuaji bila ya kupeleka wagonjwa nje ya nchi. "Serikali inachotakiwa kufanya ni kuiboresha taasisi hiyo kwa kujenga majengo mapya na kuipatia vifaa zaidi na itakapofanya hivyo itaokoa maisha ya watu na fedha nyingi ambazo zingelitumika kugharamia matibabu nje ya nchi". Mkurugenzi wa taasisi hiyo alishauri.

Mkurugenzi wa Taasisi hiyo alimweleza Dkt. Mahiga kuwa taasisi ilianzishwa miaka ya 90 kwa madhumuni ya kuokoa maisha ya watoto wenye maradhi ya moyo duniani kote, hususan katika nchi zinazoendelea. Hadi sasa imeshatoa matibabu kwa zaidi ya watoto 460,000 wenye maradhi ya moyo kutoka Afrika, Amerika, Asia na kwingineko.

Shughuli za taasisi hiyo inajumuisha kutibu wagonjwa, kutoa mafunzo kwa madaktari na wakufunzi na kusambaza madaktari katika nchi mbalimbali kuendesha upasuaji kwa kipindi maalum. Madaktari waliopewa mafunzo na taasisi hiyo wanaendelea kupata miongozo ya taasisi wanaporejea katika nchi zao kwa ajili ya kufanya matibabu.

Mhe. Waziri alipokuwa katika taasisi hiyo alipata fursa ya kuonana na Watanzania wanaosoma na wengine wanaopata matibabu ya maradhi ya moyo katika taasisi hiyo. Aidha, alioneshwa watoto wawili wanaougua maradhi ya moyo kutoka Nymmar na Romania ambao kwa mujibu wa Mkurugenzi alisema ndio wa kwanza kupokelewa kutoka nchi hizo.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Israel
10 Mei 2017

Post a Comment

0 Comments