Ticker

6/recent/ticker-posts

MEYA ATAKA KUUNDWA BARAZA LA WANAUME



Na Woinde Shizza,Arusha.

Meya wa Jiji la Arusha Kalisti Lazaro amependekeza kuundwa kwa baraza la Wanaume ambalo litasaidia kuhamasisha uwajibikaji wa wanaume kuanzia ngazi ya familia,jamii na taifa hivyo kuchochea maendeleo kwa ujumla.

Kalisti akizungumza katika Mahafali ya darasa la Wanaume lilioandaliwa na taasisi ya  wanaume ya Men At Work yenye makao yake jijini Arusha,alisema kuwa mafunzo maalumu kwa wanaume yatasaidia kupunguza wimbi la wanaume wengi kutelekeza familia na watoto pamoja na kuimarisha familia bora ambazo zitajenga taifa bora.

Alisema kuwa migogoro mingi inatokea kwenye familia nyingi kwa sababu ya wanaume wasiojielewa hivyo wanaume wakijitambua na kusimama kwenye nafasi zao familia zitapona na taifa litapona.

“kuna changamoto Sera za nchi haziongelei wanaume,sera zinawaongelea wanawake,vijana wa kike na wa kiume wanazungumziwa hata katika mikopo lakini wanaume hawajaongelewa kwenye sera” Alisema Meya

Mkurugenzi wa Taasisi ya Men At Work Maxwell Stanslaus amesema kuwa mafunzo ya wanaume yanaongeza thamani ya wanaume ,wanaume wakijitambua na kujiboresha  wanakuwa bora zaidi.

Baadhi ya Wahitimu wa darasa la Wanaume Christopher Kombe na Emanuel Vicent wameeleza kuwa darasa hilo limewasaidia kujua namna bora ya uendeshaji wa familia kwani  wanaume ni msingi wa familia na taifa.


Post a Comment

0 Comments