Ticker

6/recent/ticker-posts

KIFO CHA ASKOFU THOMAS LAIZER FAMILIA YAELEZA KILICHMUUA ASKOFU,WATAJA WOSIA MZITO ALIOUACHA



Bishop Thomas O. Laizer


FAMILIA ya marehemu  Baba skofu Thomas Laizer wa Kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania dayosisi ya kaskazini kati imesema kuwa hayati Baba askofu ameacha wosia mzito kwa waumini, wachungaji na viongozi wa kanisa hilo baada ya yeye kupita.
Akizungumza nyumbani kwa askofu huyo katika eneo la Nduruma mke wa askofu huyo Mama Maria Laizer alisema kuwa mume wake kila mara alikuwa anasisitiza kuwa kazi aliyoianzisha iendelezwe na isiharibiwe kwa vyovyote vile.
“Baba  askofu alisisitiza jambo hili hata kwa wote waliofika kumjulia hali akiwa kitandani kwake kuwa wahakikishe kuwa kazi aliyoianza inaendelezwa “alisema Mama Laizer.
Alileza kuwa alikuwa na mume wake masaa machache kabla ya kifo chake na kwamba mchana wa siku aliyoaga dunia alikuwa na hali nzuri lakini baadye hali yake ilibadilika na kuondokewa na uhai.
Alisema kuwa askofyu huyo alianza kusumbuliwa na maradhi ya kansa kwa kipindi cha miaka minne iliyopita lakini hakuweza kupata tiba stahili kwa haraka.
“Alikuwa akilalamika maumivu katika tumbo lake mara kwa mara na baadaye alizidiwa tukampeleka Nairobi akatibiwa lakini baada ya muda alianza tena kulalamika maumvu na ndipo akapelekwa India na kugundulika kuugua kansa ambayo tayari ilikuwa imesambaa mwilini”alisema Mama Laizer.
Marehemu Baba askofu Thomas Laizer ameacha mjane watoto wanne na mjukuu mmoja.
Bwana ametoa na Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe.
 

Askofu wa kanisa la kiinjili la Kilutheri Tanzania  dayosisi ya kaskazini kati Askofu Thomas lazier amefariki Dunia jioni ya leo.
Habari ambazo zimethibitishwa na katibu Mkuu wa dayosisi hiyo Israel Ole Karyongi zimesema kuwa askofu alikumbwa na mauiti majira ya saa  12 za jioni ya leo.
“Ni kweli baba Askofu amepita na tuko katika hali ya dharura ngumu na tungependa mtuachie nafasi ili tuwape taarifa juu ya msiba huu kesho”alisema Karyongi akizungumza kwa njia ya simu .
Askofu lazier ndiye  askofu wa kwanza wa na mwanzilishi wa dayosisi  hiyo ambayo awali ilikuwa ikiitwa dayossi Mkoani Arusha kabla ya mwaka juzi kubalishw ajina na kuitwa dayosisi ya kaskazini kati.
Ni msiba mkubwa mno katika Mkoa wa Arusha kutokana na askofu huyo  kupata umaarufu katika kazi zake za kiroho na kijamii husasan jamii ya kabila la wamasai.
Anatajwa kushiriki katika kuendeleza jamii hiyo kielimu kwa kubuni na kuanzisha shule zaidi ya ishirini za sekondari zikiwemo maalum kwa ajili ya watoto wa kike.
kufuatia msiba huo,Waziri Mkuu mstaafu Edward Ngoyai Lowasa amesema kuwa kanisa na jamii limempoteza kiongozi na mpigania maendeleo ya jamii kiroho na kimwili.
 “Tumepoteza kiongozi wa kiroho na kijamii,amehusika katika kuelimisha jamii kwa kuanzisha shule nyingi za Sekondari,amehusika pia ujenzi wa hospitali ya rufaa ya Arusha Lutheran Medical Center,zahanti na vituo vya afya katika vijiji  kadhaa Mkoani Arusha pamoja na hoteli ya Corridor springs”alisema Lowasa.
Aliwataka waumini wa kanisa la KKKT kuwa watulivu katika kipindi hiki kigumu baada ya kuondokewa na kiongozi wao.
"Natoa pole nyingi kwa familia ya marehemu Baba Askofu Laizer  na kanisa la KKKT kwa ujumla wake,lakini askofu Laizer atakumbukwa kwa utumishi uliotukuka katika siku za uhai wake"alisema Lowasa akihojiwa na kituo cha radio cha kitaifa cha Radio one asubuhi ya leo

Aidha aliwapongeza madaktari wa hospitali ya Seliani  kwa jitihada zao za kumsaidia baba askofu akiendelea na matibabu katika hospitali hiyo.
 

Post a Comment

0 Comments