BREAKING NEWS

Tuesday, November 5, 2013

DIWANI AMTOLEA UVIVU MWENYEKITI WA MTAA


Diwani wa kata ya Monduli mjini,(CCM),Isack Joseph maarufu kama Kadogoo “amemtolea uvivu” mwenyekiti wa mtaa wa Sabasaba uliopo ndani ya kata yake,Charles Malaika katika mkutano wa hadhara huku akimtuhumu kukwamisha utekelezaji wa ilani ya Chama cha CCM.

Mkutano huo ulifanyika hivi karibuni ndani ya kata hiyo ambapo akizungumza na wananchi mbalimbali waliohudhuria diwani huyo alimtuhumu Malaika kwamba ameshindwa kuwasilisha mpango kazi katika mtaa wake hali ambayo inakwamisha maendeleo ya kata yake.

Diwani huyo kwa jazba akiwahutubia wananchi wake alisema kuwa ni mtaa mmoja kati ya minne iliyopo ndani ya kata yake haujawasilisha mpango kazi wake wa maendeleo hali ambayo inakwamisha juhudi za maendeleo.

“Nina shaka na huyu mwenyekiti wangu wa mtaa wa Sabasaba kwa kuwa haiwezekani wewe tu usiwasilishe mpango kazi wako tofauti na wengine”alisema Joseph

Akijitetea katika mkutano huo mwenyekiti huyo alidai kuwa mwingiliano  wa majukumu ulimpelekea kutowasilisha mpango kazi huo kwa wakati huku akitoa ahadi katika mkutano huo kuwasilisha mapema iwezekanavyo.

Katika hatua nyingine,diwani huyo aliwaambia wananchi kuwa miongoni mwa masuala kama kuanzisha mfuko wa kata,kusomesha watoto wasio na uwezo sanjari na kuhakikisha wananchi  wanapata viwanja na kuanza ujenzi wa makazi ya kudumu yametekelezwa kwa asilimia 95.

Alisema kuwa katika mwaka wa fedha 2013/14 suala la ukarabati wa kituo cha mabasi cha Monduli mjini ,huduma ya maji safi na salama pamoja na ujenzi wa barabara miradi hiyo inatarajia kukamiliki kwa asilimia 100 na kuwataka wananchi wampe ushirikiano.

Share this:

Post a Comment

unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia

 
Back To Top
Copyright © 2014 MOUNT KILI NEWS. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates