Ticker

6/recent/ticker-posts

HII NDO TWASIRA YA MGOMO WA WAFANYABIASHARA KARIAKOO

 Wamiliki wamaduka walifika madukani kwao na kupiga soga bila wasi wala shida.
 Mkazi wa Dar es Salaam akizungumza na wenye duka kandokando ya barabara ya Uhuru Kariakoo jana ambao walifunga maduka yao kufuatia mgomo wa wafanyabiashara kugomea mashine za TRA ambazo wanadai zinahitilafu nyingi.
 
 Stori na wafanyakazi ziliendelea 
 Wafanyakazi wa maduka hayo walifika kazini na kukaa nje.
 Wengine walifungua maduka yao hivi.
 Wateja walipita kutafuta huduma na kukereka kabisa
 BBC ilifika Kariakoo na kuzungumza na baadhi ya wafanya biashara pamoja na wateja kupta maoni yao.
 Wateja walizunguka na kuamua kukaa chini madukani.
Duka hili wao waliamua kuendelea na biashara kwa kile walichosema kuwa hata wakiwa katika mgomo bado watalazimika kulipa kodi. Hivyo ni bora waendelee na biashara.
Jiji la Dar es Salaam hususani eneo la Kariakoo jana wafanyabishara wake katika maeneo hayo waliingia katika mgomo wa kutofungua maduka yao kupinga mashine za kutolea risiti za elektroniki (EfDs) ambazo zipo katika mfumo wa uhakiki wa ukusanyaji kodi. 

Wafanyabishara hao wakizungumza na Father Kidevu Blog, wamesema mbali na mashine hizo za EfDs lakini pia wamekuwa wakiongezewa kodi kila kukicha.

Wamesema kuwa matatizo ya mashine hizo ya kuharibika mara kwa mara, kushindwa kutoa mahesabu ya siku kwa wakati na kushindwa kuprint risiti ni kero kwao.

Pichani juu ni Wafanya biashara wa maduka ya bidhaa mbalimbali katika mitaa ya uhuru na Swahili Kariakoo, Shamun Qurban (kushoto) na mwenzake Murtaz Abbas ‘Kokole’ wakisoma gazeti nje ya maduka yao waliyoyafunga jana kufuatia mgomo wa wafanyabiashara kugomea mashine za TRA ambazo wanadai zinahitilafu nyingi.

Post a Comment

0 Comments