Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)
itafanya mkutano wake wa kawaida kwa siku mbili jijini Dar es Salaam
kuanzia tarehe 20 hadi 21 Novemba, 2013.
Ajenda za mkutano ni
kupokea, kujadili na kufanya maamuzi kuhusu: Mihutasari ya mikutano
iliyopita na yatokanayo na mikutano hiyo, taarifa ya hali ya siasa na
ripoti ya fedha.
Ajenda nyingine ni pamoja na: taarifa kuhusu
mchakato na maudhui ya mabadiliko ya katiba, taarifa ya utekelezaji wa
Programu ya CHADEMA ni Msingi na shughuli za Kanda na taarifa ya
utekelezaji wa Mpango Mkakati kuhusu maboresho.
Imesambazwa kutoka Uturuki tarehe 19 Novemba 2013 na:
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia