Ticker

6/recent/ticker-posts

MAKAMU WA RAIS KUFUNGUA MICHUANO YA SHIMMUTA NOVEMBA 19 JIJINI ARUSHA



 picha ya makamu wa rais  Samia Suluhu(picha na maktaba)
Na Woinde Shizza,Arusha

Michuano ya Shirikisho la Michezo la Mashirika ya Umma, Taasisi na Makampuni Binafsi Tanzania (SHIMMUTA), yanatarajia kuanza kutimua vumbi wiki ijayo jijini Arusha kwa kushirikisha Mikoa Yote Tanzania.


Katibu mkuu wa SHIMMUTA Award Safari alisema kuwa hadi sasa tayari mikoa kadhaa imethibitisha ushiriki wao ikiwemo wenyeji wa mashindano hayo Mkoa wa Arusha na Mikoa mingine ni Dar es salaam, Dodoma, Morogoro, Mbeya na Tanga


Tukiwa kama kamati tendaji ya SHIMMUTA tulifanya kikao tarehe saba mwezi huu pamoja na wajumbe wa timu shiriki ili kupeana miongozo na taratibu za michezo hasa tukiwa tunaboresha mapungufu yaliyojitokeza mwaka jana mkoani Tanga” alisema Safari.


Takribani michezo 12 yatafanyika ikiwa pamoja na Mpira wa Miguu, Riadha, kuvuta Kamba, Mpira wa Pete, Vishale, karata, na drafti na karata.


“Kwa mujibu wa katiba, SHIMMUTA  ipo chini ya makamu wa Raisi, hivyo mashindano ya mwaka huu tunatarajia Makamu wa Raisi Samia Suluhu atakuja kufungua mashindano hayo akiwa anachukua nafasi ya Mlezi aliyepita makamu wa Raisi Mstaafu Mohamed Ghalib Bilal” Alisema Safari.


Mashindano ya SHIMMUTA yanatarajia kuanza Novemba 19 hadi Novemba 30 mwaka huu, hivyo timu shiriki zitaanza kuwasili kuanzia tarehe 17 wakati siku inayofuata SHIMMUTA itafanya mkutano na viongozi wa timu zote zitakazofika.


SHIMMUTA ni moja ya mashirika manne yalioundwa na serikali kwa ajili ya kusimamia michezo makazini ikiwemo SHIMIWI ikiwa chini ya wizara ya kazi, SEMISEMISTA serikali za mitaa na MAJESHI ambalo linasimamiwa na Baraza la michezo la Majeshi.


Post a Comment

0 Comments