Ticker

6/recent/ticker-posts

WANAFUNZI WA VYUO KUFURAHIA HUDUMA YA KUPIGIANA SIMU BURE TOKA TIGO

Meneja Mauzo wa mkoa wa Tanga kutoka Tigo Bw.Daniel Mainoya akiongea na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali , kuhusu uzinduzi wa kifurushi kilichoboreshwa cha University Pack kutoka Tigo katika Uwanja wa chuo cha Utumishi wa Umma, Kange, mjini Tanga.
Mwanafunzi kutoka chuo cha Utumishi wa Umma, Kange,mjini Tanga, Bi.Stella Mwakiliku akiongea na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali  kuhusu vipi wanafunzi wamekikubali kifurushi hicho kilichoboreshwa cha University Pack kutoka Tigo.

  1. Mwanafunzi kutoka chuo cha Utumishi wa Umma, Kange, Bw.Albert Risala akiongea na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali kuhusu vipi wanafunzi wamekipokea kifurushi hicho kilichoboreshwa cha University Pack kutoka Tigo.
      Kikundi cha sarakasi  kikitumbuiza wanafunzi  katika uzinduzi wa kifurushi cha University pack kilichoboreshwa katika uwanja wa chuo cha Utumishi wa Umma,Kange, mjini Tanga.
Msanii wa kizazi kipya Roma Mkatoliki akiwatumbuiza wanafunzi wa chuo cha Utumishi wa Umma,Kange, mjini Tanga,katika uzinduzi wa kifurushi cha University pack kutoka Tigo kilichoboreshwa.




 Kampuni ya simu za mkononi ya Tigo imezindua kifurushi maalum kinacho wawezesha wanafunzi, ambao ni wateja wa Tigo, kuweza kupigiana simu bure.

Huduma hii imeboreshwa zaidi baada ya kifurushi hicho kwa jina maarufu kama Tigo Uni Pack kuzinduliwa mwaka jana, ukilinganisha na kifurushi cha zamani, kifurushi hichi kipya cha wiki kitawapatia wanafunzi wepesi wa kujiunga wakiwa popote ndani ya nchi, hii ni kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari na kampuni ya Tigo leo.

Kinachohitajika ili wanafunzi waweze kutumia huduma hii,ni kuhakiki kwamba wamesajiliwa kama wateja wa Tigo katika Vyou vyao, ujumbe huo ulisema.

Akizungumzia kifurushi hicho kilichoboreshwa, Meneja wa Bidhaa kutoka Tigo Edwin Mgoa,alisema kifurushi hicho cha Uni Pack, kinadhirisha vipi Tigo inavyowasaidia wanafunzi kwa ajili ya kuwawezesha kuweza kupata huduma za mtandao za maisha ya kidijitali.
Baadhi ya huduma za kidijitali zinazotelewa na Tigo ni upatikanaji wa muziki bila kikomo kwa kupitia huduma ya Tigo Music, Facebook ya Kiswahili, Tigo Pesa App, Tigo Backup- huduma inayowawezesha wateja wa Tigo kuweza kurudisha simu na  zinapoibiwa au kupotea.

Kujisajili kwa kifurushi cha Uni Pack, mwanafunzi atahitajika kupiga *148*01*20#, namba ambazo kwa mujibu wa taarifa hiyo, imejumuisha vifurushi vingine muruwa kutoka Tigo.


Post a Comment

0 Comments