Ticker

6/recent/ticker-posts

YEMBA KUGOMBEA USPIKA

 
 
ALIYEKUWA mgombea urais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania kupitia Chama cha ADC, Chief Lutayosa Yemba, ametangaza kugombea kiti cha Spika wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania kupitia chama cha ADC.

Chief Yemba, ameyasema hayo leo jijini Arusha, alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari akitoa tathimini ya uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 25 mwaka huu, pamoja na kutathimini uchaguzi wa jimbo la Arusha ambao unatarajiwa kufanyika Desemba 13 mwaka huu.

Amesema baada ya kuanguka kwenye urais, sasa anaelekeza nguvu zake kwenye Usipika, ambako ana uhakika wa kushinda kuwa ana sifa na vigezo  na ana imani atashinda kwa kuwa anaungwa mkono na wabunge wengi wakiwemo wa CCM.

Aidha,ametumia fursa hiyo kuwashukuru wananchi wa Arusha kwa kumpigia kura 200 kwenye uchaguzi mkuu uliopita licha ya chama chake kuwa ni kichanga na sasa anafanya kazi ya kukijenga mkoani humo.

Amesema uchaguzi mkuu umekwishana tayari mgombea wa ccm, Dakta John Magufuli, ndie rais na ADC, inamtambua na inampongeza kwa ushindi huo na hivyo itashirikiana nae na Pia ADC ingelimtambua mgombea yeyote ambae angelishinda kwenye uchaguzi mkuu Oktoba 25 mwaka huu.

Kuhusu marudio ya uchaguzi wa Zanzibar, Chef Yemba, amesema ADC, itashiriki kwenye uchaguzi huo ambao ulifutwa kutokana na kugubikwa na kasoro nyingi na kutabiri kuwa ADC, itakuwa ni sehemu ya serikali ya Zanzibar kwa kuwa itapata ushindi mkubwa .

Ameiomba serikali ya mapinduzi Zanzibar, kuvunja tume ya taifa ya uchaguzi na kuunda nyingine  itakayosimamia haki  kwa wagombea wote na kuepuka kasoro zilizojitokeza zisijirudie na kuvuga uchaguzi .

Amesema kwenye uchaguzi uliopita mawakala wa ADC,  walizuiliwa kuingia kwenye vituo vya uchaguzi kwa ajili ya kuhakiki zoezi zima la uchaguzi mkuu na kushangazwa na vituko vya matokeo Pemba ambapo  yeye Chief Yemba,alipata kura nyingi zaidi kuliko mgombea urasi wa Zanzibar, Hamad Rashid, ambae Pemba ndio ngome yake alipata kura 114 lakini ilijaziwa  kura 4 wakati yeye akipata kura 90.

 Kuhusu uchaguzi wa ubunge jimbo la Arusha, ameipa ccm 38% Chadema 30 na ACT wazalendo 6%, na kusema kuwa huo ni kwa mjibu wa utafiti alioufanya wa kuzungumza na makundi mbalimbali ya wananchi wakiwemo waztu wazima vijana na wanawake.

Ameongeza kuwa hata hivyo ushindi utaamuliwa na kundi la waswahili ambalo mpaka sasa halijatoa mwelekeo wa nani wamuunge mkono.

Yemba, amesema ADC katika uchaguzi huo haifungamani na chama chochote bali inahitaji mbunge  na sio chama cha siasa .

Amesema kinachohitaji kwa Arusha ni kupata  mbunge bora makini atakaezungumzia namna ya kuboresha huduma za afya ,elimu  na sio kusuguana na serikali ili Arusha iweze kusonga mbele katika maendeleo.

“Umefika wakati wanasiasa kuachana na siasa za misuguano kati ya wanasiasa na viongozi wa serikali ili Arusha iweze kusonga mbele”alisema yemba.

Ameongeza kuwa mbunge wa Arusha, anayetetea kiti chake ameshindwa kufanya mabadiliko  ya maendeleo na badala yake amejenga chama chake ,wananchi wanahitaji mbunge wa kuwasemea na sio chama cha mtu.

Yemba, Amesema ADC,ilikuwa inategemea kuona wananchi wakiandamana kupinga bei ya maji kupanda licha ya kuandamana kwa ajili ya kukosekana kwa maji pekee.

Post a Comment

0 Comments