Ticker

6/recent/ticker-posts

JUMUIYA YA WAZAZI CCM WILAYA YA ARUSHA WAKABIDHI MAGODORO 25 KATIKA MAHABUSU YA WATOTO ARUSHA

picha ikionyesha wa kwanzakushoto ni Afisa ustawi wa jamii ambaye pia ni msimamizi wa mahabusu ya watoto mkoa wa Arusha Mussa Mkamate akiwa anabadilishana jambo na baadhi ya wajumbe wa Jumuiya ya wazazi CCM wilaya ya Arusha mara baada yakukabidhi magodoro kama msaada wa mahabusu hayo
Na Woinde Shizza , Arusha
Kamati ya utekeleza  ya wazazi wa CCM wilaya ya Arusha  leo wamekabidhi jumla ya magodoro 25 katika mahabusu ya watoto iliyopo jijini hapa ikiwa ni ahadi walioiweka ya kusaidia baadhi ya changamoto zilizopo katika mahabusu hiyo.
Akizungumza mara baada ya kukabidhi magodoro hayo mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo ambaye pia ni meneja masoko wa Radio ya Triple A iliopo jijjini Arusha  Phidecia Mwakitalima alisema kuwa hii ni mara ya tatu wao kama kamati ya  wazazi wa wilaya kukabidhi msaada huo kwani mara ya kwanza walishatoa chakula na mashuka kwa ajili ya watoto hao na sasa hivi wameamua kuwaletea msaada wa magodoro.
Alisema kuwa magodoro hayo 25 yametokana na msaada ambao wao kama kamati ya wazazi waliuomba kwa wadau mbalimbali ambapo katika wadau hao kampuni ya magodoro ya Tanform iliopo arusha iliwaunga mkono na kuamua kuwapa magodoro hayo kwa ajili ya watoto hao wa mahabusu ya watoto Arusha.
Aidha Phidecia alimalizia kwa kutoa wito kwa wadau mbalimbali ,wafanyabishara ,viongozi  pamoja na wananchi  kujijengea tabia ya kutembelea mhabusu mbalimbali za watoto zilizopo hapa nchini ili  kuweza kugundua changamoto walizo nazo watoto hao na kuweza kuwasadia kuzitatua ikiwa ni pamoja na kuwapa baadhi ya mahitaji ambayo watoto hao walioko mahabusu hawayapati  pamoja na kutatua kero walizo nazo.
Naye mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wilaya ya Arusha  Ally Mtumwa alisema kuwa juhudu za jumuiya ya wazazi CCM wilaya ya Arusha hazitaishia hapo  kwani huu ni mwanzo wataendelewa kuwasadia watoto wa mahabusu hii pamoja na watoto wengine wanao ishi katika mazingira magumu na wale yatima waliopo ndani ya mkoa wa Arusha.
Alisema wao kama wazazi wanaguswa sana na baadhi  ya matatizo yanayowapata watoto hao wanaoishi katika mahabusu hii ya watoto pamoja na wale wanaoishi katika mazingira magumu hivyo watajitaidi kwa kila njia kuwasadia .
“hii sio mara ya kwanza  kuwasadia watoto hawa na wala sio watoto hawa tu tunawasaidia  na pia atutaishia hapa tutaendelea kuwasaidia watoto hawa sisi kama wazazi adi pale tutakapoona sasa watoto hao wanaishi katika hali nzuri kama wale watoto wana wazazi wanaoishi majumbani kwao.
Kwa upande wake katibu wa wazazi CCM  wilaya Arusha Rehema Mohamed alisema kuwa  mara ya kwanza walipotembelea katika mhabusu haya walikuta magodoro yamechakaa ,eneo limechakaa,watoto wanaishi katika mazingira magumu ,vyoo vya mahabusu hiyo vilikuwa vibovu pamoja na mahabusu hiyo kutokuwa na chakula cha kutosha kwa ajili ya watoto hao lakini wao kama jumuiya walishirikiana kutafuta wadau   ambao wamejitokeza kusaida kutatua baadhi ya changamoto ikiwa ni pamoja na kupeleka chakula,mashuka ambayo hayakuwepo sasa ivi wamempata huyu ambaye aliwapelekea magodoro na wao wameyachukuwa na kuyakabidhi katika mahabusu hiyo.
“pia  naomba sana serekali ,pamoja na mahakama kwa ujumla kuangalia usikilizaji wa kesi za watoto hawa kwani kuna baadhi ya watoto wameshakaa ndani ya mahabusu hiyo kwa muda mrefu lakini kesi zao azisikilizwi ,na ambazo zinasikilizwa azitolewi ukumu kwa wakati na zikitolewa ukumu watoto hao wanatakiwa kufungwa badala ya kupewa adhabu tunaomba sana serekali hii iangalie sana kwa makini swala hili “alisema Rehema.
Aidha alitolea mfano mmoja wa mtoto(12) ambaye alishitakiwa kwa kosa la kuiba simu  lakini ilifikia sehemu mwenye simu alimsamehe ,na alivyopelekwa mahakamani motto huyo  alikiri kosa  na kutolewa ukumu afungwe miaka miwili  ,kitu ambacho ni sio kizuri kwani sheria inasema mtoto kama huyo anatakiwa kupewa adhabu na sio kufungwa.

Post a Comment

0 Comments