Ticker

6/recent/ticker-posts

MTOTO ABDUL AOMBA MSAADA KWA WASAMARIA WEMA WA MATIBABU KWENDA NJE YA NCHI

 picha ikionyesha mtoto  Abdul Hussein mwenye Umri wa Miaka 7 mkazi wa daraja Mbili jijini Arusha anayesumbuliwa na maradhi ya Mtindio wa Ubongo pamoja na ulemavu wa viungo anaishi Kwa mateso makubwa kwani tangu azaliwe hajawahi kuamka ,kuona wala kusikia akiwa anapewa maziwa na mama yake Ashura Hussen ,mama huyu anaomba msaada wa kifedha kwa wananchi ,viongozi wa dini ,wabunge pamoja na Rais ili apate fedha za kumpeleka  mtoto wake  nje ya nchi kwa ajili ya matibabu  (picha na Woinde Shizza,Arusha)
 baadhi ya waandishi wa habari wakikabidhi vitu ambavyo wamechanga kwa ajili ya kumsaidia mama huyo ambaye ameacha kazi kutokana na kumlea mtoto huyo tangu amzae 
 Theodora Mrema mwandishi wa Stax Tv akikabidhi sabuni ikiwa ni moja ya michango iliyotolewa na waandishi wa habari wa mkoa wa Arusha 
 Geofrey Steven mwandishi wa Radio 5 akiwa anakabidi baadhi ya nguo zilizotolewa na waandishi wa habari waliomtembelea mtoto huyo
hawa ni baadhi ya waandishi wa habari wa mkoa wa Arusha waliojitolea kumtembelea mtoto Abdul  anaesumbuliwa na ugonjwa wa mtindio wa ubongo

Na Woinde Shizza,Arusha 

Mtoto Abdul Hussein mwenye Umri wa Miaka 7 mkazi wa daraja Mbili jijini Arusha anayesumbuliwa na maradhi ya Mtindio wa Ubongo pamoja na ulemavu wa viongo  anaishi Kwa mateso makubwa kwani tangu azaliwe hajawahi kuamka ,kuona wala kusikia.

Mama mzazi wa mtoto Huyo Ashura Hussein Amesema kuwa mtoto wake huyo amekuwa na matatizo tangu azaliwe na aligundulika kuwa na tatizo LA mtindio wa Ubongo akiwa na umri wa miaka miwili

Mtoto wangu Siku nilipojifunga katika hospitali ya Temeke,Dar Siku ya kwanza hakuweza kulia ama kunyonya kama ilivyo kwa watoto wengine.

"Madaktari walimwekea mpira wa maziwa ,baadae baada ya mwaka  alianza kunyonya na ilipofika mwaka mmoja na nusu alikuwa akining'ata anapokuwa akinyonya ndipo madaktari wakaniambia ni mwachishe kumnyonyesha ndipo nikamwachisha na akaanza kutumia mpira tangu hapo  "Amesema mama Mzazi

Aidha Alisema kuwa alianza kumpa  chakula na mpira na  alipofikisha umri wa miaka miwili alikumbwa na tatizo  kutapika kila anapokula chakula tatizo lililoendelea hadi sasa ambapo kwa sasa anapewa chakula kupitia mrija Kwa kutumia bomba la sindano lakini pindi anapokula akikaa baada ya muda mchache amekuwa akirudisha chakula chote kwa kutapika  

"kutokana na matatizo haya kwakweli mimi nilikuwa nesi imenibidi niache sifanyi kazi yoyote nakaa tu hapa nyumbani   kwani siwezi hata kwenda kuajiriwa maana siwezi kwenda na mtoto  hivyo naishi maisha ya shida sana kusema kweli jamani angalau hata ningekuwa hata na kaofisi ka kuniingizia riziki "aliseama Ashura  mama mzazi wa Abudul

Mama Huyo amewaomba wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa serikali wabunge na Rais John Magufuli kuweza kumsaidia ili apate fedha Kwa ajili ya kumpatia matibabu nje ya nchi mtoto huyu .

Hata hivyo  wanahabari Jiji LA  Arusha wamemtembelea mtoto huyo nakumpatia msaada kidogo wa zaidi ya sh, 300,000 pamoja na mavazi  kwa ajili ya mtoto huyo  .



Post a Comment

0 Comments