Ticker

6/recent/ticker-posts

SHAHIDI AIELEZA MAHAKAMA JINSI RAIA WA CHINA ALIVYOTUMIA JINA LA KAMPUNI YAKE KUCHUKUA FEDHA BONNITE

Shahidi wa kwanza katika kesi ya madai inayomkabili raia wa nchini China,Xu Ling ameieleza mahakama ya kwamba raia huyo alitumia jina la kampuni yao kufanya kazi za ujenzi katika kampuni ya Bonnite Bottlers Ltd iliyoko mjini Moshi na kisha kuchukua malipo ya kiasi cha zaidi ya sh,400 milioni.
Shahidi huyo ambaye ni mkurugenzi wa kampuni ya ujenzi ya Woodmender Co,Ltd ,Amaniel Ndossa alitoa ushahidi wake mwishoni mwa wiki iliyopita katika kesi hiyo nambari 2 ya mwaka 2017  mbele ya hakimu mkazi,Janeth Mawole wa mahakama ya hakimu mkazi Moshi.
Akiulizwa swali na wakili wa upande wa mashtaka ,Issa Mavura kwamba makubaliano baina ya kampuni yake na raia huyo yalikuwaje shahidi huyo aliiambia mahakama hiyo kwamba walikubaliano na Xu Ling  atumie jina la kampuni yake na kisha amlipe asilimia 10 ya fedha katika kazi aliyoifanya Bonnite Bottlers Ltd.
Shahidi huyo aliieleza mahakama hiyo kwamba katika makubaliano hayo pia walikubaliana kwamba Xu Ling ambaye pia ni mkurugenzi wa kampuni ya Li Jun Development Ltd kwamba atalipa kodi zote za mamlaka ya mapato(TRA) mara akishapokea malipo ya kazi hiyo .
Akijibu swali aliloulizwa na wakili upande wa utetezi,Isaac Samson kwamba alijuaje ya kwamba mteja wake amelipwa malipo ya kazi hiyo shahidi huyo alisema kwamba walipata taarifa kutoka mamlaka ya mapato(TRA) mkoani Arusha kwamba Xu Ling alifika kulipa kodi ya ongezeko la thamani(VAT).
Mbele ya mahakama hiyo shahidi huyo alisema ya kwamba anatambua ya kwamba kuna taarifa iliyofunguliwa mbele ya jeshi la polisi mkoani Arusha kuhusu raia huyo kughushi baadhi ya nyaraka za malipo za kazi hiyo zikiwemo baadhi ya risiti za malipo(invoice).
Mara baada ya kumaliza kutoa ushahidi wake hakimu Mawole alihairisha kesi hiyo hadi Mei 17 mwaka huu ambapo shahidi mwingine upande wa mashtaka atafika mbele ya mahakama hiyo kuwasilisha ushahidi wake.

Post a Comment

0 Comments