ofisa wa TMA ambaye nesi
Prisca Mwandaji akiongea na wananchi wakati wa ufunguzi wa zoezi la upimaji wa magojwa
yasioambukiza na yale yanayoambukiza hususa ni upimaji wa ugonjwa wa
kifua kikuu Pamoja na maambukizi ya virusi vya Ukimwi(HIV)ili kuwasaidia
wananchi wa monduli Kujua afya zao.
mmoja wa daktari kutoka chuo cha kijeshi monduli akiwa anampa
ushauri mmoja wa mama wa kimasai aliyehudhuria kupima afya yake
madaktari kutoka chuo cha kijeshi cha monduli (TMA) wakiwa wanatoa
huduma ya upimaji wa magojwa yasioambukiza na yale yanayoambukiza
hususa ni upimaji wa ugonjwa wa kifua kikuu Pamoja na maambukizi ya
virusi vya Ukimwi(HIV) bure ili kuwasaidia wananchi wa wilaya ya mondul
kaimu mganga mkuu halmashauri ya wilaya ya monduli Sakina
Msangi akiongea na wananchi waliouthuria kupima
Na Woinde Shizza, Monduli
Zaidi
ya wananchi 470 tarafa ya mto wa mbu wilayani monduli mkoani Arusha
wamepatiwa huduma ya upimaji wa magonjwa yanayoambukiza na Yale
yasioambukiza bure ili kuwawezesha wananchi hao kutambua afya zao
Huduma
hiyo ambayo inatolewa na madaktari kutoka Katika chuo cha kijeshi cha
monduli (TMA) inatarajiwa kuwafikia wananchi waliopo Katika kata
,Tarafa na vijiji vyote vya wilaya ya Monduli.
Akizungumzia
zoezi hilo Katika viwanja vya mto wa mbu ofisa wa TMA ambaye ni nesi
Prisca Mwandaji alisema kuwa wao Kama madaktari kutoka chuo cha kijeshi
cha monduli (TMA) wameamua kutoa huduma hii ya upimaji WA magojwa
yasioambukiza na yale yanayoambukiza hususa ni upimaji wa ugonjwa wa
kifua kikuu Pamoja na maambukizi ya virusi vya Ukimwi(HIV)ili kuwasaidia
wananchi wa monduli Kujua afya zao.
"hii
ni moja ya kazi zetu wanajeshi kusaidia wananchi hivyo basi Susi kama
madkatari tumeamua kujitoleakupima wananchi bure hawachangii hata kidogo
na huduma hii tunaitoa katika tarafa zote za wilaya ya monduli na
magonjwa ambayo tunapima na kushuri wananchi wanaokuja hapa kupima ni
HIV Pamoja na kifua kikuu maana haya nimgonjwa mabaya na yanayoambukiza
hivyo ndio maana tunawasisi tiza wananchi wapime ili wajue afya zao
ukiangalia na huduma tunatoa bure"alisema Mwandaji
Aidha
alisema Kuwa hadi sasa walishapima tarafa Moja ambayo ni makuyuni
ambapo jumla ya wananchi 350 na pia hapa mto wa mbu tumeshapima wananchi
470 na bado wanaendelea kuwapima.
"kwakweli
kwa upande WA muitikio ni mkubwa maana kwanza hadi sasa kwa hapa mto wa
mbu tulishapita malengo tulitarajia kupima watu 450ila tumeshapita adi
sasa tumeshapima watu 470 na tunaendelea hivyo kwakweli muitikio ni
mkubwa mno kiukweli "alisema Mwandaji
Aidha
alimalizia kwakutoa wito kwa wananchi kuwa na desturi ya kupima Mara
kwa Mara ilikujua afya zao zipoje kwani iwapo atapima na kujikuta
mgonjwa ni vizuri maana ataanza kupata tiba na dawa mapema kabla ya
tatizo kuwa kubwa akitolea mfano ugonjwa wa kifua kikuu ambao
unaambukizwa kwa njia ya hewa, alimalizia kwakutaja kauli mbiu yao ya
ugonjwa wa kifua kikuu kuwa ni"tuwe mstari wa mbele kupambanua na
kutatua maambukizi ya kifua kikuu.
Kwa
upande wake kaimu mganga mkuu halmashauri ya wilaya ya monduli Sakina
Msangi alisema kuwa nimuimu kupima afya Pamoja na kupata elimu ya afya
ilikujua maisha yetu yanaendeleaje kiafya
Aidha
alisema kuwa kwa sasa ivi wilaya ya monduli maambukizi ya virusi vya
ukimwi yamepungua kwa kiasi kikubwa huku akitoa takwimu kuwa mwaka
2016-2017 kulikuwa na asilimia 6% ya walioambukizwa lakini kwa mwaka
2017 kuanzia January adi December imepungua na kufika asilimia 4% ndio
waliopata maambukizi ya virusi vya ukimwi hivyo imepungua kwa asilimia
2%.
Aliwapongeza chuo cha
kijeshi cha TMA kwa jinsi walivyoamua kutoa huduma Hizi za upimaji bure
kwa wananchi wao kwani wameonyesha kuwa ni kwajinsi gani wao kama
watumishi wa serikali wanawajali wananchi wao kwa kuwapima bure na
kuwapa elimu ya upimaji afya zao na kutambua faida za kupima afya zao
mara kwa Mara na hasara za kutokupima afya zao.
0 Comments
unashauriwa kutoa maoni muda na wakati wowote na kama unahabari yeyote unaruhusiwa kututumia